Jana tumeisikia ngoma mpya ya Dayna Nyange aliyomshirikisha Nay Wa Mitego‘Nitunze’ leo kupitia story za kiburudani zaidi za 255 amezungumzia ishu ya wasanii wa kike kuwashirikisha wasanii wa kiume kwenye ngoma zao.
Dayna amesema inategemea na msanii anaimba kitu gani, idea nyingi wanaimba kuhusu mapenzi kwa hiyo wanaamua kuwashirikisha wasanii wa kiume ili kuwakilisha pande zote mbili.
Kumbe Dayna ana list ya wasanii wake anaowaangalia sana kwa sasa.. anayaangalia mafanikio yao pia, yuko Diamond, AY, Ommy Dimpoz, Nay Wa Mitego… KamtajaVanessa Mdee pia kwa upande wa wasanii wa kike.

Kuhusu ishu hiyohiyo ya Linex, Meneja wa Tip Top Connection Babu Tale amesema kukataliwa kwa video hiyo na vituo hivyo ni jambo la kawaida kwa sababu wana vigezo vyao wanavyoangalia kama ilivyo kwa vituo vingine hapa nchini, wakikuta video haina vigezo hivyo hawawezi kuicheza.

Rapper Young Dee amesema ameshindwa kuachia ngoma yake mpya kama alivyoahidi kutokana na tour yake ya ‘Ongea na Young Dee’ anayoendelea kuifanya kwa kuzunguka mikoa mbalimbali.. kwa sasa anaangalia jinsi ya kukaa na Management yake na kuamua siku ya kuiachia ngoma hiyo.
Bonyeza play kusikiliza story zote za 255 leo…
0 maoni:
Chapisha Maoni