• This is default featured slide 1 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

  • This is default featured slide 2 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

  • This is default featured slide 3 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

  • This is default featured slide 4 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

  • This is default featured slide 5 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

Jumamosi, 22 Machi 2014

Benki ya Dunia kuudhamini Mradi wa Inga

Mitambo mikongwe kwenye bwawa la Inga ambalo Benki ya Dunia imekubali kulidhamini
Mitambo mikongwe kwenye bwawa la Inga ambalo Benki ya Dunia imekubali kulidhamini
Benki ya Dunia imeridhia kutoa dola milioni 73 kuisaidia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika mpango wake wa ujenzi wa bwawa la Inga, ambalo ndilo kubwa kabisa duniani la kuzalisha umeme kutumia nguvu ya maji.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Benki ya Dunia, fedha hizo dola milioni 73 zikichanganywa na zengine dola milioni 33 kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika, zitasaidia kufadhili utafiti wa kiufundi kuchunguza hali ya mazingira karibu na eneo la bwawa na kuhakikisha mradi huo ni endelevu.
Fedha hizo pia zitasaidia kuzindua usimamizi wa maendeleo ya Inga unaojitegemea ambao unatarajiwa kufuata mfumo mzuri wa Kimataifa katika kuuendesha mradi huo, na hata kuteua mashirika binafsi yatakayosaidia katika kuufadhili zaidi mradi wa bwawa la Inga.
Bwawa la kuzalisha umeme la Inga ndilo kubwa zaidi duniani

Hata hivyo, Benki ya Duinia imeiorodhesha Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kama moja ya maeneo 10 yaliyo magumu kufanyia biashara. Kwa miongo kadhaa sasa miradi ya kulipanua bwawa hilo la Inga imeshidnwa kutokana na migogoro na vita vinavyotokea mara kwa mara nchini humo, huku wanamazingira wakionya kuwa mipango ya mabwawa makubwa inajulikana kwa kucheleweshwa kwa muda mrefu na kuwa na gharama kubwa.
Benki ya Dunia inakadiria kuwa Kongo itakuwa na uwezo wa kutoa takribani jigawati 100 ya nguvu za umeme, ikiwa ni ya tatu duniani baada ya China na Urusi. Lakini ni asilimia 9 pekee ya idadi ya raia wa Congo milioni 65 walio na uwezo wa kupata umeme huku katika sekta ya madini inayochangia kiwango kikubwa cha uchumi wa nchi hiyo uhaba wa umeme ukisalia kikwazo kikubwa.
Ramani hii inaonyesha njia ndefu ya kusafirisha umeme kutoka Inga hadi Afrika Kusini
Lakini kwa sasa mpango wa Afrika Kusini kununua umeme kutoka Inga, umefufua mazungumzo ya mradi huo mkubwa. Kwa sasa mashirika matatu makubwa ya kimataifa yanapigania kandarasi ya kujenga bwawa hilo linalojulikana kama Inga ya tatu, na kuuza nguvu ya umeme inayopatikana inayokadiriwa kuwa megawati 4,800.
Hii ni takriban mara tatu ya nguvu ya umeme iliyokuwa inatolewa kwa mabwawa mawili ya Inga, yalioko kwa muda mrefu sasa na yalioharibiwa kutokana na madeni ya serikali ya Congo na wafanyabiashara walioogopa kuwekeza katika miradi hiyo.
Kwa upande wake Waziri Mkuu wa Congo, Augustin Matata Ponyo, ametoa taarifa akisema kuwa mradi wa Inga ni mradi unaoweza kuibadilisha Afrika katika karne hii ya 21.
Wakati huo huo kundi moja liitwalo International Rivers limeukosoa mpango huo kwa kutokuwa na manufaa zaidi kwa raia wa nchi hiyo na kutoa wito kwa Benki ya Dunia kufadhili mipango midogo ya kawi kama ya umeme wa kutumia jua ambayo limesema haitadhuru mazingira kwa kiwango kikubwa.
dw.de/swahili
Share:

Benki ya Dunia kuudhamini Mradi wa Inga

Mitambo mikongwe kwenye bwawa la Inga ambalo Benki ya Dunia imekubali kulidhamini
Mitambo mikongwe kwenye bwawa la Inga ambalo Benki ya Dunia imekubali kulidhamini
Benki ya Dunia imeridhia kutoa dola milioni 73 kuisaidia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika mpango wake wa ujenzi wa bwawa la Inga, ambalo ndilo kubwa kabisa duniani la kuzalisha umeme kutumia nguvu ya maji.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Benki ya Dunia, fedha hizo dola milioni 73 zikichanganywa na zengine dola milioni 33 kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika, zitasaidia kufadhili utafiti wa kiufundi kuchunguza hali ya mazingira karibu na eneo la bwawa na kuhakikisha mradi huo ni endelevu.
Fedha hizo pia zitasaidia kuzindua usimamizi wa maendeleo ya Inga unaojitegemea ambao unatarajiwa kufuata mfumo mzuri wa Kimataifa katika kuuendesha mradi huo, na hata kuteua mashirika binafsi yatakayosaidia katika kuufadhili zaidi mradi wa bwawa la Inga.
Bwawa la kuzalisha umeme la Inga ndilo kubwa zaidi duniani

Hata hivyo, Benki ya Duinia imeiorodhesha Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kama moja ya maeneo 10 yaliyo magumu kufanyia biashara. Kwa miongo kadhaa sasa miradi ya kulipanua bwawa hilo la Inga imeshidnwa kutokana na migogoro na vita vinavyotokea mara kwa mara nchini humo, huku wanamazingira wakionya kuwa mipango ya mabwawa makubwa inajulikana kwa kucheleweshwa kwa muda mrefu na kuwa na gharama kubwa.
Benki ya Dunia inakadiria kuwa Kongo itakuwa na uwezo wa kutoa takribani jigawati 100 ya nguvu za umeme, ikiwa ni ya tatu duniani baada ya China na Urusi. Lakini ni asilimia 9 pekee ya idadi ya raia wa Congo milioni 65 walio na uwezo wa kupata umeme huku katika sekta ya madini inayochangia kiwango kikubwa cha uchumi wa nchi hiyo uhaba wa umeme ukisalia kikwazo kikubwa.
Ramani hii inaonyesha njia ndefu ya kusafirisha umeme kutoka Inga hadi Afrika Kusini
Lakini kwa sasa mpango wa Afrika Kusini kununua umeme kutoka Inga, umefufua mazungumzo ya mradi huo mkubwa. Kwa sasa mashirika matatu makubwa ya kimataifa yanapigania kandarasi ya kujenga bwawa hilo linalojulikana kama Inga ya tatu, na kuuza nguvu ya umeme inayopatikana inayokadiriwa kuwa megawati 4,800.
Hii ni takriban mara tatu ya nguvu ya umeme iliyokuwa inatolewa kwa mabwawa mawili ya Inga, yalioko kwa muda mrefu sasa na yalioharibiwa kutokana na madeni ya serikali ya Congo na wafanyabiashara walioogopa kuwekeza katika miradi hiyo.
Kwa upande wake Waziri Mkuu wa Congo, Augustin Matata Ponyo, ametoa taarifa akisema kuwa mradi wa Inga ni mradi unaoweza kuibadilisha Afrika katika karne hii ya 21.
Wakati huo huo kundi moja liitwalo International Rivers limeukosoa mpango huo kwa kutokuwa na manufaa zaidi kwa raia wa nchi hiyo na kutoa wito kwa Benki ya Dunia kufadhili mipango midogo ya kawi kama ya umeme wa kutumia jua ambayo limesema haitadhuru mazingira kwa kiwango kikubwa.
dw.de/swahili
Share:

HOTUBA YA JK,WAKATI WA KULIHUTUBIA BUNGE MAALUM LA KATIBA

Mheshimiwa Samuel Sitta, Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba;
Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi;
Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar;
Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Mheshimiwa Anne Semamba Makinda; Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano;
Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho, Spika wa Baraza la Wawakilishi na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalum la Katiba ;
Mheshimiwa Rashid Othman Chande, Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Othman Makungu, Jaji Mkuu wa Zanzibar;
Viongozi Wakuu Wastaafu;
Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba;
Waheshimiwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba;
Wageni waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Pongezi
Nakushukuru sana Mheshimiwa Mwenyekiti kwa kunipa fursa ya kuja kuzungumza na Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge letu Maalum la Katiba katika siku hii muhimu na ya kihistoria kwa nchi yetu. Nimekuja kuwatakia heri na naungana na Watanzania wenzetu wote kuwaombea baraka za Mwenyezi Mungu, ili muweze kuifanya kazi yenu kwa utulivu, hekima, umakini mkubwa na kuimaliza kwa salama na kwa mafanikio yanayoyatarajiwa na Watanzania.
Natoa pongezi nyingi kwako na kwa Makamu wako kwa kuchaguliwa kwenu kuongoza Bunge hili maalumu na la kihistoria. Ushindi mkubwa mliopata ni kielelezo tosha cha imani kubwa na matumaini waliyonayo Wajumbe wenzenu kwenu. Matumaini yao ndiyo matumaini ya Watanzania wote, kwamba mtaliongoza vizuri Bunge hili, ili liweze kutimiza kwa ufanisi mkubwa jukumu lake muhimu sana katika historia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Niruhusu pia niwapongeze kwa dhati Wajumbe wote wa Bunge Maalum la Katiba kwa bahati ya aina yake waliyopata ya kutunga Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Fursa hii hutokea mara chache sana katika historia ya nchi yo yote na watu wake. Mkifanikiwa kuipatia nchi yetu Katiba nzuri majina yenu yataandikwa kwa wino wa dhahabu, katika kumbukumbu za historia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ni matarajio ya Watanzania kuwa mtatunga Katiba itakayokubalika na wengi. Katiba inayotekelezeka. Katiba itakayoimarisha Muungano wetu kwa kuondoa changamoto zilizopo sasa. Katiba itakayoipa nchi yetu mfumo bora wa kuongoza na kuendesha mambo yetu. Katiba itakayoimarisha umoja, upendo, ushirikiano na mshikamano miongoni mwa wananchi wa Tanzania, licha ya tofauti zao za asili za upande wa Muungano na maeneo watokako, au tofauti za jinsia, rangi, kabila, dini na ufuasi wa vyama vya siasa. Katiba itakayodumisha amani, usalama na utulivu nchini. Katiba itakayostawisha zaidi demokrasia, haki za binadamu, utawala wa sheria, utawala bora na kudhibiti maovu.
Na, mwisho ingawaje siyo mwisho kwa umuhimu, Katiba itakayoweka mazingira mazuri kwa uchumi wa nchi kukua, na wananchi wengi kunufaika sawia na maendeleo yatayopatikana.
Historia ya Katiba Nchini
Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wajumbe;
Hii itakuwa mara ya tatu tangu kuzaliwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Aprili 26, 1964, kwa nchi yetu kuwa na mchakato wa kutunga Katiba mpya. Mara ya kwanza ilikuwa mwaka 1965 ilipotungwa Katiba ya Muda na mara ya pili ni mwaka 1977 ilipotungwa Katiba ya Kudumu tuliyonao sasa. Tofauti na mara mbili zilizopita, safari hii mchakato unahusisha watu wengi zaidi. Wananchi wameshiriki moja kwa moja kutoa maoni yao kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, na ndio watakaofanya uamuzi wa mwisho kuhusu Katiba mpya kwa kura ya maoni. Wananchi pia walipata nafasi ya kuchagua Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya yaliyojadili Rasimu ya Kwanza ya Katiba. Pia walipata nafasi ya kutoa maoni yao kupitia Mabaraza ya Katiba ya taasisi. Katika Bunge hili wapo wananchi 201 kutoka makundi mbalimbali.
Katika mchakato wa kutunga Katiba za mwaka 1965 na 1977 kulikuwapo Tume za Kuandaa Rasimu na Bunge Maalum la Katiba kama ilivyo katika mchakato huu. Hata hivyo, kwa Katiba zilizopita Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano pekee ndio waliounda Bunge Maalum. Safari hii Bunge Maalum linajumuisha Wabunge, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na wananchi 201 wanaotoka kwenye jamii, wakiwakilisha asasi na makundi mbalimbali ya Watanzania kutoka Zanzibar na Tanzania Bara. Mchakato wa sasa utaishia kwenye kura ya maoni itakayoshirikisha wananchi wote wa Tanzania wanaoruhusiwa kupiga kura. Michakato iliyopita iliishia Bunge Maalum pekee.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Tangu kutungwa kwake, tarehe 25 Aprili, 1977, mpaka sasa Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 imefanyiwa mabadiliko takriban mara 14. Mabadiliko hayo yalitokana na kufanyika au kutokea kwa mabadiliko muhimu ya kiuchumi, kisiasa na kijamii katika nyakati mbalimbali hapa nchini na katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Kwa ruksa yako naomba nitaje baadhi ya mabadiliko yaliyofanywa:-
Mabadiliko ya 1979 yaliunda Mahakama ya Rufani ya Tanzania kufuatia kufa kwa Mahakama ya Rufani ya Afrika Mashariki baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977.
Mabadiliko ya mwaka 1980 yalifanyika baada ya kutungwa kwa Katiba ya Zanzibar, hivyo kulazimu Katiba hiyo kutambulika kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano
Mabadiliko ya mwaka 1984 yaliweka utaratibu wa ukomo wa vipindi vya Urais ambao haukuwepo kabla ya hapo. Aidha, masuala ya Haki za Binadamu (Bill of Rights) yaliingizwa kwa mara ya kwanza katika Katiba. Vilevile, Mahakama ya Rufani ya Tanzania na mambo mengine ya iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliongezwa katika Orodha ya Mambo ya Muungano.
Mwaka 1992, yalifanyika mabadiliko yaliyoanzisha Mfumo wa Vyama Vingi vya Siasa badala ya ule wa Chama kimoja uliokuwepo tangu 1965. Pia utaratibu wa uchaguzi wa Rais na Wabunge ulirekebishwa ili uendane na mfumo wa vyama vingi vya siasa. Vilevile utaratibu wa kuwa na viti maalum vya wanawake katika Bunge ulianzishwa. Wakati ule ilikuwa asilimia 15 ya Wabunge wote. Aidha, kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu Bunge lilipewa mamlaka ya kumwajibisha Rais na Waziri Mkuu kupitia kura ya kutokuwa na imani.
Mabadiliko ya mwaka 1994 yaliweka mfumo mpya wa kumpata Makamu wa Rais kupitia Mgombea Mwenza.
Mwaka 2000 na 2005, pamoja na mambo mengine yalifanyika mabadiliko yaliyopanua wigo wa Haki za Binadamu na kuongeza uwakilishi wa wanawake.
Umuhimu wa Mabadiliko ya Katiba
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kufanyika kwa mabadiliko hayo kunathibitisha utayari wa Serikali kufanya mabadiliko kila ilipoonekana inafaa kufanya hivyo. Pamoja na kufanya yote hayo na Serikali kuwa na msimamo huo, kumekuwepo na madai yaliyokuwa yanajirudia ya kutaka Katiba ya Tanzania iandikwe upya. Wako watu walioimithilisha Katiba yetu na nguo yenye viraka vingi mno kiasi kwamba ingefaa kununua mpya badala ya kuendelea kuivaa.
Madai ya kutaka Katiba mpya yalipazwa sauti baada ya kuanza kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa. Wapo waliokuwa wanadai Katiba mpya kwa imani, eti kwamba, itawawezesha kuishinda CCM. Lakini, si hayo tu, hata katika mchakato wa Serikali zetu mbili kushughulikia kero za Muungano, imedhihirika kuwa baadhi ya changamoto zilikuwa zinahitaji mabadiliko ya Katiba ili kuzipatia ufumbuzi wa uhakika na wa kudumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kwa kutambua ukweli huo na baada ya kushauriana na kukubaliana na viongozi wenzangu wakuu wa Chama tawala na Serikali zetu mbili wakati ule, ndipo tarehe 31 Desemba, 2010, nikatangaza dhamira ya kuanzisha mchakato wa kutunga Katiba mpya. Nilieleza siku ile kuwa katika mchakato huo tutakuwa na ushirikishwaji mpana wa wananchi wa Tanzania kwa makundi yao ya jinsia, dini, siasa na shughuli wazifanyazo kujipatia riziki na kwa maeneo wanayotoka katika pande zetu mbili za Muungano.
Mchakato wa Katiba Mpya
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Tarehe 16 Machi, 2011 Baraza la Mawaziri liliridhia kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya kuliongoza taifa katika mchakato wa kutunga Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tarehe 18 Novemba, 2011 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Kwa mujibu wa Sheria hiyo, mchakato wa kutunga Katiba Mpya ulikuwa unaanza kwa kuunda Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Tume hiyo imepewa jukumu la kusikiliza maoni ya wananchi mmoja mmoja na kwa makundi yao ya maslahi, taasisi zao na kupitia Mabaraza ya Katiba. Mwishowe Tume imetakiwa kutengeneza Rasimu ya Katiba mpya itakayofikishwa kwenye Bunge Maalum la Katiba kujadiliwa na Katiba mpya kutungwa. Mchakato wa Katiba utahitimishwa kwa wananchi kupiga kura ya maoni ya kuamua kama wanaikubali au kuikataa Katiba mpya.
Tarehe 6 Aprili, 2012 nilifanya uteuzi wa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kuwaapisha tarehe 13 Aprili, 2012. Tume ilianza kazi tarehe 2 Mei, 2012 na kuikamilisha kwa mafanikio, hatua zote zilizoihusu na kukabidhi kwangu na kwa Rais wa Zanzibar, Taarifa ya Tume na Rasimu ya Katiba tarehe 30 Desemba, 2013. Kitendo cha Mwenyekiti wa Tume, Mheshimiwa Joseph Warioba kuwasilisha Rasimu hiyo mbele ya Bunge hili tukufu tarehe 18 Machi, 2014, kinahitimisha rasmi kazi ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Kazi inayofuatia ni ya Bunge hili kujadili, kuamua na kutunga Katiba mpya. Baada ya hapo Katiba mpya itafikishwa kwa wananchi kwa uamuzi wa mwisho kwa njia ya kupiga kura ya NDIYO au HAPANA.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Rasimu ya Katiba ilichapishwa kwenye gazeti la Serikali na magazeti mengine yanayosomwa na wananchi kama ilivyoagizwa katika Kifungu cha 20(2) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Pamoja na hayo, Taarifa ya Tume na Rasimu ya Katiba viliwekwa wazi kwenye tovuti ya Tume kwa kila mtu kusoma. Inafurahisha kuona kuwa watu wengi wameisoma Taarifa ya Tume na Rasimu ya Katiba na kumekuwa na mjadala mpana kuhusu nyaraka zote hizo muhimu. Watu wengi wametoa maoni yao na wanaendelea kufanya hivyo. Kwa maoni yangu hili ni jambo jema sana na ni kielelezo thabiti kuwa demokrasia imestawi na inazidi kuota mizizi Tanzania. Pia, kwamba, Watanzania wako huru kushiriki na kutoa maoni yao kwa mambo yanayowahusu.
Pongezi kwa Tume
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kwa mara nyingine tena narudia kutoa pongezi za dhati kwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya uongozi wa Mheshimiwa Jaji Joseph Warioba akisaidiwa na Mheshimiwa Jaji Augustino Ramadhani, kwa kazi kubwa na nzuri waliyofanya. Kazi yao haikuwa rahisi hasa ukizingatia ukubwa wa nchi yetu, wingi wa watu wake, utitiri wa taasisi na pigo la kumpoteza Mjumbe mwenzao muhimu Dkt. Sengondo Mvungi aliyetangulia mbele ya haki katikati ya mchakato.
Pamoja na hayo, kwa bidii kubwa Wajumbe wa Tume wameweza kutembelea mikoa yote nchini na kuwafikia watu 351,644 waliotoa maoni yao kwa mdomo na kwa maandishi. Halikadhalika, walipokea na kuchambua maoni 772,211 kutoka kwa wananchi na taasisi mbalimbali. Baada ya kupokea maoni ya wananchi, kufanya utafiti na kwa kutumia maarifa na uzoefu wao, Wajumbe wakafanya kazi ngumu, kuliko yote, ya kutengeneza Rasimu ya Katiba iliyoko mbele ya Bunge hili. Ni kweli kwamba Wajumbe hawakuweza kuwafikia wananchi wote wa Tanzania, lakini wameweza kuwafikia wananchi wengi, ambao kwa kiasi kikubwa wanawakilisha taswira na mitazamo mipana ya jamii yetu.
Baadhi ya Masuala Yaliyojitokeza Katika Mjadala wa Mapendekezo ya Tume
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Tume imefanya kazi nzuri, yenye thamani kubwa na ya manufaa kwa taifa la Tanzania. Rasimu imeandikwa vizuri na kwa weledi wa hali juu. Tume imetoa mapendekezo ambayo kwa kiasi kikubwa yanahuisha na kuboresha Katiba ya nchi yetu, kwa namna ya pekee. Katiba inayopendekezwa, imejumuisha dhana na mambo kadhaa mapya yanayokwenda vyema na wakati tulionao na kuweka msingi mzuri kwa huko mbele tuendako. Kwa taratibu za kawaida za marekebisho ya Katiba tuliyonayo, isingekuwa rahisi kuingiza mambo mengi mapya kiasi hiki.
Wajumbe Wana Kazi Kubwa
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Waheshimiwa Wajumbe;
Rasimu ya Katiba ni kitabu kikubwa kilichosheheni mambo mengi. Kina kurasa 106, sura 17 na ibara 271. Wajumbe wa Bunge hili mnatakiwa kusoma na kuelewa vizuri kila kilichoandikwa ili muweze kufanya uamuzi ulio sahihi. Mnawajibika kuchambua kwa kina na umakini mkubwa kila kilichomo, sura kwa sura, ibara kwa ibara, sentensi kwa sentensi na hata neno kwa neno. Hamna budi kujiridhisha kuhusu uandishi wa vifungu vya Rasimu ya Katiba na kufaa kwa dhana mbalimbali zilizoingizwa na kujengeka katika Rasimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kile ambacho Wajumbe mtaona kinastahili kuboreshwa au kurekebishwa au kufutwa msisite kufanya hivyo ili Watanzania wapate Katiba iliyo bora. Msipofanya hivyo kuna hatari ya kupata Katiba ambayo ni ngumu kuitekeleza. Aidha, tunaweza kuwa na Katiba ambayo itanung'unikiwa na watu wengi na kusababisha madai ya kutaka ifanyiwe marekebisho muda mfupi baada ya kupitishwa. Bunge hili linao wajibu maalum wa kuzuia balaa hilo lisitokee katika nchi yetu. Ngazi mbalimbali zilizowekwa katika mchakato huu ni kama chujio la kuepusha hali hiyo isitokee. Kile ambacho hakikuonekana katika hatua moja kitaonekana katika hatua inayofuata na kurekebishwa. Nawaomba fursa mliyonayo muitumie vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Nimekwishaeleza kuwa moja ya jambo mnalotegemewa kufanya ninyi wenzetu mliopewa dhamana ya kutunga Katiba ya nchi yetu ni kujiridhisha na uandishi wake. Yapo maoni yaliyotolewa kuhusu uandishi ambayo naomba myatafakari na kuamua ipasavyo. Kwa mfano, kuna baadhi ya vifungu vya Katiba vinayopendekezwa vimekuwa na mambo mengi mno kuliko inavyostahili Katiba kuwa (too prescriptive). Pia kuna mawazo kwamba baadhi ya mambo hayangetakiwa kuwa katika Katiba bali yawe kwenye Sheria zinazotafsiri utekelezaji wa Katiba yenyewe.
Yako mambo yaliyotajwa kwenye Katiba ambayo yanatakiwa kuelezwa wazi kuwa mtu hatakwenda mahakamani kuidai Serikali impatie (non justiciable). Mambo yaliyotajwa kwenye Katiba ni mazuri na yanavutia, lakini lazima yaendane na uwezo wa nchi na uchumi wake kuhimili. Simaanishi kwamba tuyatoe kwenye Katiba, bali yabakie kama dhamira pale uwezo wa nchi utakaporuhusu yatekelezwe. Tusipofanya hivyo, kuna hatari ya Serikali kujikuta inalaumiwa au hata kufikishwa mahakamani kila wakati kwa madai ya jambo moja au jingine ambayo haina uwezo nayo. Ni muhimu sana mambo kama hayo muyatazame ili tusije kuwa na Katiba ambayo ni ngumu kutekeleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Yapo pia maoni kuwa baadhi ya vifungu vina upungufu katika uandishi wake, hivyo kuhitaji kufanyiwa marekebisho. Isipofanyika hivyo kunaweza kuwepo athari na nyingine zinaweza kuwa mbaya. Kwa mfano, Ibara ya 2 ya Rasimu inayotambulisha eneo na mipaka ya nchi yetu. Ibara hiyo inasomeka kuwa "Eneo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni eneo lote la Tanganyika likijumuisha sehemu yake ya bahari na eneo lote la Zanzibar likijumuisha sehemu yake ya bahari".
Maelezo hayo yameacha kutambua, kwa upande wa Tanzania Bara, sehemu yetu ya maziwa na mito ambayo ni kubwa sana. Kwa nini tuache kuitaja? Je hatutoi nafasi kwa nchi tunazopakana nazo siku moja wakaja kupora sehemu zetu hizo na sisi kukosa utetezi kwa kuwa hata Katiba yetu haikuyatambua maeneo hayo kuwa ni yetu? Hili ni jambo kubwa ambalo Bunge hili lazima mlirekebishe. Wakati ndiyo huu hakuna mwingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Jambo jingine kuhusu uandishi ni mgongano kati ya pendekezo la msingi la Tume la kuwa na muundo wa Serikali tatu na majukumu ya Serikali ya Muungano ambayo kimsingi ni majukumu ya Serikali za nchi washirika. Katika Rasimu hii malengo ya taifa yameainishwa na Serikali ya Muungano inatakiwa kuhakikisha kuwa malengo hayo yanatekelezwa na itoe taarifa Bungeni. Katika mfumo wa Serikali tatu unaopendekezwa na Tume masuala yahusuyo uchumi na maendeleo ya jamii kama vile kukuza kilimo, ufugaji, uvuvi, viwanda, biashara, pembejeo, elimu, hifadhi ya jamii na kadhalika yako chini ya mamlaka ya Serikali za nchi washirika. Mamlaka ya Serikali ya Muungano ni kwa mambo saba tu yafuatayo:- Katiba na Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano, Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano, Uraia na Uhamiaji, Sarafu na Benki Kuu, Mambo ya Nje, Usajili wa Vyama vya Siasa, Ushuru wa Bidhaa na Mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na Mambo ya Muungano.
Kwa Rasimu kupendekeza muundo wa Serikali tatu na kuipa Serikali ya Muungano majukumu ambayo haina mamlaka nayo, ni kuzusha utata na migongano kati ya Serikali ya Muungano na nchi washirika. Mkichagua mfumo wa Serikali tatu, inawalazimu muyaondoe mambo hayo kwani Serikali ya Muungano haistahili kuyatekeleza na wala haina uwezo wa kuweka masharti kwa Serikali za nchi washirika kwa mambo yaliyo kwenye mamlaka ya nchi hizo. Lakini kama mtaamua tuendelee na muundo wa Serikali mbili, mambo haya mazuri yanatekelezeka na Serikali ya Muungano bila ya matatizo. Katika uandishi wa Rasimu Utumishi katika Serikali ya Muungano haumo katika Orodha ya Mambo ya Muungano. Ni lazima liwemo. Hayo ni baadhi tu ya masuala yahusuyo uandishi katika Rasimu. Naamini mkiisoma Rasimu kwa makini mnaweza kuyagundua mengineyo.
Dhana Mpya
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Katika Rasimu kuna dhana mpya na mambo mapya kadhaa yaliyoingizwa ambayo yanabadili utaratibu wa sasa wa uendeshaji wa nchi na mambo mbalimbali. Nawaomba mfanye uchambuzi wa kina kwa kila kinachopendekezwa na kujiridhisha kuhusu kufaa kwake na manufaa yake. Fanyeni hivyo ili tujihakikishie kuwepo kwa mambo mazuri na uendeshaji mzuri wa shughuli katika taifa letu changa.
Mambo ni mengi na kwa ufinyu wa muda sitaweza kuyazungumzia yote. Niruhusuni nizungumzie baadhi ya dhana na mambo mapya yaliyomo katika Rasimu. Jambo la kwanza, kwa mfano, linahusu Ibara ya 128 (2)(d) inayoleta dhana ya "Mbunge kupoteza Ubunge iwapo atashindwa kufanya kazi za Mbunge kwa miezi sita mfululizo kutokana na maradhi au kizuizi ndani ya gereza".
Watu hawana tatizo na Mbunge kuwa kizuizini ndani ya gereza kama amepatikana na hatia Mahakamani na kuhukumiwa kifungo. Lakini, isijekuwa yuko rumande kwa tuhuma akisubiri kesi kusikilizwa. Je akija kuonekana hana hatia na kuachiliwa? Naungana na wale wanaoshauri kuwa jambo hili lifafanuliwe vizuri na kutambua Mbunge kutiwa hatiani na kupata adhabu ya kifungo cha kipindi hicho. Ni bora ifanyike hivyo sasa ili kuondoa mikanganyiko. Hakuna haja ya kusubiri mpaka jambo hili lije kufafanuliwa baadaye kwa Sheria itakayotungwa na Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kwa upande wa mtu kupoteza Ubunge kwa sababu ya "kuugua kwa miezi sita mfululizo" ni maoni ya watu wengi kuwa huu ni ukatili ambao haustahili kufanywa na Katiba. Kuugua ndiyo ubinadamu na wakati mwingine Mbunge anaweza kupata ajali akiwatumikia wananchi wa Jimbo lake. Anaweza kuugua kwa miezi sita au zaidi na kupona kabla ya kipindi chake cha Ubunge kufika mwisho. Kwa nini awekewe ukomo wa miezi sita? Katiba ya mwaka 1977 tunayotumia sasa haina sharti hilo. Watu wanauliza hoja na haja ya kuwa na sharti hili kwenye Katiba mpya ni ipi? Wanasema kwa kweli anachostahili Mbunge huyu kufanyiwa ni kuuguzwa afya yake iimarike ili aendelee kutumikia watu wake, na siyo kupoteza uongozi wake. Tusiwatie watu kishawishi cha kukatiza matibabu ili kukwepa sharti hilo. Ni vyema jambo hili mkalitazama kwa makini, na muone kama linastahili kuwepo au hapana.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Katika Rasimu hii imeingizwa dhana mpya ya kuweka ukomo wa vipindi vitatu kwa Wabunge. Tena mapendekezo haya hayasemi vipindi vitatu mfululizo au la!. Jambo hilo limezua mjadala motomoto katika jamii. Ni vizuri mkajiridhisha juu ya sababu za msingi na manufaa ya kufanya hivyo hapa Tanzania. Mazoea yetu na ya kwingineko duniani ni kuweka ukomo kwa Wakuu wa Nchi kwa sababu nzuri na rahisi kuzielezea. Lakini, kuwawekea ukomo Wabunge ni jambo jipya na huenda Tanzania tukawa wa kwanza. Nashawishika kuungana na wale wanaopendekeza kuwa pengine ni mapema mno kuanzisha utaratibu huo hapa kwetu.
Nachelea kuwa tutainyima nchi yetu fursa ya kupata watu wenye maarifa na uzoefu mzuri wa uongozi kwa nafasi ya Ubunge au kwa nafasi za uongozi wa Taifa bila ya sababu za msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Jambo lingine jipya linalopendekezwa na Tume ni utaratibu wa kumuondoa Mbunge katikati ya kipindi chake cha uongozi. Kwa hoja linaonekana kuwa jambo jema lakini naomba athari zake mzitafakari vizuri. Kuna hatari ya kuanzisha misuguano kwenye Majimbo na kuwaacha Wabunge wasifanye kazi zao kwa utulivu bali wawe wanajihami dhidi ya wapinzani wao kuwatengenezea fitna za kuwatoa. Utaratibu unaopendekezwa wa Chama chake kujaza nafasi ya Mbunge inapokuwa wazi katika mazingira hayo nao unaweza kuwa ndicho kichocheo kikubwa cha vuguvugu la kumuondoa Mbunge. Walioshindwa kwenye kura ya maoni wanaweza kufanya kazi ya kuwachimba wenzao mpaka waondoke. Jipeni muda wa kupima faida na hasa thamani inayoongezwa na kuanzisha utaratibu huo. Naomba tujiridhishe kama jambo hili jipya lina tija. Hivi kupewa nafasi kila miaka mitano kurudi kwa wananchi hakutoshi kumuondoa Mbunge ambaye watu wamemchoka?
Muundo wa Muungano
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Jambo lingine kubwa lililopendekezwa na Tume ambalo limevuta hisia za karibu watu wote nchini linahusu muundo wa Muungano wetu kuwa wa Serikali tatu badala ya mbili za sasa. Pendekezo hili limezua mjadala mkubwa tangu lilipotolewa katika Rasimu ya kwanza na kurudiwa katika Rasimu ya pili. Wakati mwingine mjadala umekuwa mkali na wa hisia kali kwa kila upande.
Kwa kweli hili ndilo jambo kubwa kuliko yote katika Rasimu kwa sababu linapendekeza kuanzishwa kwa muundo na mfumo mpya wa kuendesha nchi yetu. Hii ndiyo agenda mama ya Bunge hili ambayo kila Mtanzania anasubiri kwa hamu uamuzi wenu utakuwa upi. Ombi langu kwenu ni kuwa watulivu mnapojadili suala hili. Epukeni jazba ili mfanye uamuzi ulio sahihi. Lazima mtambue uamuzi usiokuwa sahihi kwa jambo hili una hasara kubwa. Tunaweza kupoteza kitu tulichokijenga kwa gharama kubwa kwa nusu karne iliyopita. Tanzania inaweza kuwa nchi iliyojaa migogoro na matatizo mengi ambayo hatunayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wajumbe;
Kama alivyoeleza Mwenyekiti wa Tume Mheshimiwa Jaji Joseph Sinde Warioba, mara kadhaa, mjadala au madai ya kutaka muundo wa Serikali tatu si jambo jipya. Ulikuwepo hata wakati wa mazungumzo ya kuunganisha nchi zetu mbili mwaka 1964. Ulikuwa kiini cha kuchafuka kwa hali ya hewa ya kisiasa Zanzibar mwaka 1984. Muundo huu uliwahi kupendekezwa na Tume ya Nyalali mwaka 1992, ndiyo hoja ya G55 mwaka 1993 na umependekezwa pia na Tume ya Jaji Kisanga ya mwaka 1998. Lakini mara zote hizo mapendekezo hayo hayakukubaliwa.
Waasisi wa taifa letu, yaani Mwalimu Julius Nyerere, aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Tanganyika wakati ule na Sheikh Abeid Amani Karume, aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar wakati ule, waliamua kuchagua Muungano wa Serikali mbili tulionao sasa. Walitoa sababu mbili kuu: "ni muundo unaoihakikishia Zanzibar kuwa haimezwi na Tanganyika; na pia unaiepusha Tanganyika kubeba mzigo mkubwa wa kugharamia Serikali ya Tanganyika na ile ya Muungano".
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Natambua kuwepo kwa rai ya kutaka Mwalimu Nyerere asitumiwe katika mjadala huu. Nionavyo mimi ni vigumu kuacha kujadili fikra za Mwalimu Nyerere na Sheikh Karume katika jambo hili. Wao ndiyo wa mwanzo kujadili na kukubaliana kuwa mfumo wa Serikali mbili ndiyo bora kwa nchi yetu. Iweje leo tunapozungumzia kuubadili, mawazo yao yawe hayafai kutumika au hata kuzungumzwa. Hivi hasa mawazo ya nani pekee ndiyo bora zaidi kutumika? Tutakuwa hatuutendei haki mjadala huu na sisi wenyewe tunaoshiriki katika mchakato huu. Rai yangu kwenu ni kuwa mzitazame hoja zote kwa marefu na mapana yake ili mpime kama zipo sababu za kuubadili muundo wa sasa wa Muungano wa Serikali mbili na kuleta wa Serikali tatu. Na, kama zipo mabadiliko hayo yaweje! Lazima mfanye uamuzi kwa utambuzi na hoja zenye mashiko. (you must make an informed decision).
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Tume imetoa sababu mbili kubwa za kupendekeza muundo wa Serikali tatu. Sababu ya kwanza ni kwamba ndiyo matakwa ya Watanzania wengi kote Zanzibar na Tanzania Bara. Inaeleza kuwa idadi kubwa ya Watanzania waliotoa maoni, yaani asilimia 60.2 wa kutoka Zanzibar wanaunga mkono muundo wa Serikali ya Mkataba, na asilimia 61.3 wa kutoka Tanzania Bara wanaunga mkono muundo wa Serikali tatu. Sababu ya pili ni kwamba muundo huo unatoa majawabu ya uhakika na endelevu kwa changamoto za muundo wa sasa wa Serikali mbili zinazonung'unikiwa na watu wa pande zetu mbili za Muungano.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Sababu hizi mbili kuu zilizotolewa na Tume zimezua mjadala mkali katika jamii. Wapo wanaokubaliana na Tume na wapo wasiokubaliana nayo. Wapo wanaosema Tume imesema kweli kwamba Watanzania wengi wanaunga mkono muundo wa Serikali tatu, hivyo muundo wa Serikali tatu hauepukiki. Ndiyo matakwa ya wengi hivyo msemo wa Kiswahili usemao wengi wape uheshimiwe.
Lakini wapo wanaodai kuwa takwimu za Tume hazionyeshi ukweli huo. Wanasema kuwa taarifa ya Tume imeonesha kuwa Watanzania waliotoa maoni yao kwa Tume kwa mdomo na maandishi walikuwa 351,664. Kati yao ni wananchi 47,820 au sawa na asilimia 13.6 ndiyo waliokerwa na muundo wa Muungano hivyo wakauzungumzia. Wananchi 303,844 au sawa na asilimia 86.4 muundo wa Muungano kwao halikuwa tatizo, ndiyo maana hawakuuzungumzia kabisa. Wanahoji kuwa iweje leo asilimia 13.6 ya Watanzania wote waliotoa maoni wageuke kuwa ndiyo Watanzania walio wengi!
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Wanasema pia, kwamba mbona Taarifa ya Tume yenyewe, kuhusu takwimu (uk. 66 na 67), inaonesha kwamba kati ya hao watu 47,820 waliotoa maoni kuhusu Muungano, ni watu 17,280 tu ambao ni sawa na asilimia 37.2 ndiyo waliotaka muundo wa Serikali tatu, asilimia 29.8 walitaka Serikali mbili, asilimia 25.3 walipendekeza Serikali ya Mkataba na asilimia 7.7 walipendekeza Serikali moja. Hii hoja ya Watanzania wengi kutaka Serikali tatu msingi wake upi?
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Takwimu za Tume (uk. 57) zinaonyesha, vilevile kuwa Tume ilipokea maoni 772,211. Kati ya hayo asilimia 10.4 tu ndiyo yaliyozungumzia muundo wa Muungano na asilimia 88.6 hayakuzungumzia Muungano bali mambo mengine. Hivyo basi wanahoji pia kwamba kama muundo wa Muungano ungekuwa ni jambo linalowakera Watanzania wengi, lingedhihirika kwenye idadi ya watu waliotoa maoni na kwenye idadi ya maoni yaliyotolewa. Yote hayo hayakujitokeza. Waliouzungumzia Muungano walikuwa asilimia 13.6 tu ya watu wote waliotoa maoni na maoni yanayohusu Muungano yalikuwa asilimia 10.4 ya maoni yote. Hivyo basi, wanauliza "usahihi wa hoja ya Watanzania wengi kutaka Serikali tatu uko wapi?"
Changamoto za Muundo wa Serikali Mbili
Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wajumbe;
Kama nilivyokwishagusia awali, sababu ya pili ambayo Tume inatoa kuhusu kufaa kwa muundo wa Serikali tatu ni kwamba mfumo huu unajibu changamoto nyingi za muundo wa Serikali mbili. Tume imeainisha vizuri changamoto za muundo wa Serikali mbili. Kwa upande wa Zanzibar wanalalamikia kile kinachoitwa Tanzania Bara kuvaa koti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hivyo kutumia mamlaka ya Serikali ya Muungano kujinufaisha yenyewe. Fursa hiyo Zanzibar hainayo. Aidha, wanasema mipaka na mamlaka ya Serikali ya Muungano kwa mambo ya Muungano, na kwa mambo ya Tanzania Bara haijaainishwa vizuri ikaeleweka. Wazanzibari pia, wanazungumzia mkanganyiko kuhusu ugawanaji wa mapato, na jinsi ya kuchangia shughuli za Muungano baina ya Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Vilevile, wanalalamikia Rais wa Zanzibar kuondolewa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
Aidha, kuna malalamiko kuwa orodha ya mambo ya Muungan
Share:

Jumatano, 19 Machi 2014

Wanafunzi wamkata panga mwalimu wao

Bunda. Wanafunzi wawili wa Shule ya Sekondari ya Kibara, wilayani Bunda  wamefikishwa mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Bunda wakikabiliwa na shtaka la kumshambulia na kumjeruhi kwa panga mwalimu mkuu wa shule hiyo.
Ilielezwa kuwa wanafunzi hao walimjeruhi mwalimu huyo baada ya kutaka kurejeshewa fedha zao za ada kwa vile hawakuwa na mpango tena wa kuendelea na masomo shuleni hapo.
Hata hivyo imeelezwa kuwa uongozi wa shule hiyo ulipinga azma hiyo ya wanafunzi kuacha shule na kurejeshewa fedha zao.
Mwendesha Mashtaka Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Masoud Mohamed aliwataja washtakiwa hao wanaosoma kidato cha tatu kuwa ni Amosi Shirima (22) na James Athuman (22).
Washtakiwa kwa pamoja wanadaiwa kutenda kosa hilo Machi 17 mwaka huu.
Mohamed alidai kuwa siku ya tukio, saa  5:00 asubuhi, washtakiwa hao kwa pamoja walimvamia mkuu wa shule, aliyetajwa kwa jina la Awadh Said wakati akiwa ofisini kwake shuleni hapo.
Baada ya kuvamia ofisini kwake, watuhumiwa walimshambulia sehemu mbalimbali za mwili kwa panga na kusababisha majeraha makubwa.
Masoud alisema baada ya mwalimu kuona anashambuliwa, alipiga kelele za kuomba msaada kabla ya watu kujitokeza na kuwakamata watuhumiwa na baadaye kuwapeleka kituo cha polisi.
Ilielezwa mahakamani hapo kuwa hali ya mwalimu huyo siyo nzuri na anaendelea kupata matibabu hospitalini alikolazwa.
Washtakiwa kwa pamoja wamekana shtaka lao mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Safina Semfukwe.
 Hakimu Semfukwe aliamuru washtakiwa kurudishwa rumande mpaka kesi yao itakapotajwa Aprili Mosi, 2014.
Share:

Sitta yu msalabani, kuongoza Bunge Maalumu la Katiba?

Dar es Salaam. Mkanganyiko pekee na uliobakia kwa Watanzania  wakiwamo wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba ni viporo kwenye kanuni za 37 na 38, vinginevyo hali ya hewa ndani ya Bunge hilo imetulia.
Wajumbe wa Bunge hilo wapo tayari kuanza kibarua cha kwanza cha kujadili Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya, kazi ambayo  hakuna shaka ndiyo iliyowaweka Dodoma.
Hata hivyo, kabla ya mwenyekiti mteule Samuel Sitta kushinda kinyang’anyiro  cha kuongoza Bunge hilo wiki iliyopita, chama chake, CCM kimekuwa kikionekana kuwa na mkakati wa nguvu wa kushawishi na hatimaye kupitisha mapendekezo na matakwa yake, yakiwamo ya Serikali mbili.
Sitta ambaye amechaguliwa kwa asilimia 86.5 ya kura za wajumbe ana mtihani mzito aliobebeshwa mabegani ukiwamo wa kutetea msimamo wa chama chake au kuukana.
Akisaidiwa na Samia Suluhu Hassan ambaye naye amechaguliwa kwa asilimia 74, wawili hawa wana kibarua mbele yao.
Yeye (Sitta), ni muumini wa Serikali mbili kama ilivyo CCM, ingawa inaaminika kuwa amebadili msimamo kutoka ule wa awali wa Serikali tatu.
Tayari, ameahidi mbele ya wajumbe kulinda muungano kwa njia yoyote ile kupitia rasimu hiyo.

Mtego mpya kwake ndani ya Bunge ni imani kubwa ambayo  wajumbe hao wanayo kwake kwani bila kujali itikadi zao wamempitisha kuwa mwenyekiti wao kwa idadi ya kura 487, sawa na asilimia 86.5.
Hii ni ishara ya kumwamini kwamba, atahakikisha anatetea masilahi ya Watanzania wote badala ya chama chake.
Matumaini hayo yanakuja baada ya kujijengea uaminifu mkubwa kupitia uongozi wake wa Bunge la Tisa la Jamhuri ya Muungano kupitia kaulimbiu yake ya ‘kasi na viwango’.
Wapo  Watanzania wanaosema kuwa nafasi hiyo kwa Sitta inaweza kumjengea umaarufu ama kumwondolea imani kwao, endapo hatakuwa mwangalifu katika kuliongoza Bunge hilo.
Share:

HIVYO NDIVYO ILIVYOKUWA JANA KATIKA SIKU YA MAJI HUKO MJINI IRINGA.

OY_7_6a8aa.jpg
Pichani ni madiwani wa manispaa ya Iringa, waliohudhuria semina iyo iliyofanyika leo katika ukumbi wa Maji-IRUWASA.
Na Riziki Mashaka, Iringa
Semina ya Madiwani wa Manispaa ya Iringa, wakiendelea na semina inayoendeshwa na mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Iringa mjini katika ukumbi wa maji uliopo katika majengo ya ofisi za mamlaka hiyo, madiwani wa IRUWASA katika manispaa hiyo walihudhuria semina hiyo inayolenga kuboresha huduma ya maji kwa wakazi wa manispaa hiyo, maudhui ya semina hiyo ni uhakika wa maji na nishati ili kuimarisha sekta ya maji pia kutoa huduma bora kwa wakazi wa manispaa ya Iringa.
OY_1_73334.jpg
Diwani mmoja akitoa hoja zake katika mkutano huo.
OY_5_4212f.jpg
Mgeni rasmi katika semina hiyo ambaye pia ni mwenyekiti wa bodi ya IRUWASA, Bw. Muhongole akitoa hoja mbele ya madiwani waliohudhuria semina hiyo.
Semina hiyo iliendeshwa na Eng, Martin Lusindiko ambaye pia ni meneja mtendaji upande wa mitambo ya IRUWASA na mgeni rasmi katika semina hiyo ambaye pia ni mwenyekiti wa bodi ya IRUWASA, Bw. Muhongole, alihudhuria na kutoa mchango wake katika semina hiyo ya wiki ya maji. Madiwani hao walikaa katika meza moja na kujadili mambo muhimu ili kukuza sekta hiyo kama vile kujadili gharama inayoingia na kutoka kwa kila mwezi, matengenezo ya miundombinu mfano utengenezaji wa mabarabara na mabomba yanayosambaza maji katika maeneo husika ya manispaa hiyo, IRUWASA inatumia huduma ya maji yanayozalishwa na nguvu ya nishati na maeneo ya mwinuko maji usambazwa pia kwa kutegemea nguvu ya nishati.
OY_6_1cde3.jpg
Bw. M. Lusindiko ndiye aliyekuwa mwendeshaji mkuu wa semina hiyo ambaye pia ni meneja mtendaji upande wa mitambo ya IRUWASA akiwa anatoa ufafanuzi katika semina hiyo.
Madiwani hao walijadili mambo mengi katika mipango mikakati yao ya kuboresha huduma za IRUWASA kama maeneo ya gharama na kuainisha viwango vya pesa vinavyoikabili mamlaka hiyo ; gharama za kuzalisha maji (umeme, dawa, mishahara na mengine), maslahi ya watumishi, utawala, kutangaza biashara na kibenki.
OY_8_0cb58.jpg
Mkurugenzi mtendaji wa IRUWASA, Bw. Martin Mfugale alipokuwa anajibu baadhi ya maswali ya madiwani katika semina hiyo.
Semina hiyo ilishuhudia madiwani wengi wakitoa malalamiko yao kutoka katika maeneo yao ya usimamizi ambayo yanapelekea mamlaka hiyo kutumia fedha nyingi na hatimaye kutumia gharama kubwa kinyume na pato linaloingia, kwa mujibu wa mamlaka hiyo, shilingi milioni 300 na kidogo ndiyo kipato kinachoingia kwa mwezi wakati gharama za uendeshaji zinafika mpaka shilingi milioni 500 hivyo ni dhahiri kuwa mamlaka hiyo inatoa pesa nyingi kuliko zinazoingia.
Mamlaka hiyo bado ipo katika mpango mkakati wa kupandisha bili ili kufidia kiasi cha fedha zilizopotea kutokana na gharama zisizokudiwa kama wizi, na upotevu wa matumizi yasiyo sahihi yaliyosababisha matumizi makubwa ya fedha katika sekta hiyo, hivyo EWURA (Consumer Consulatative Council) ndio wenye mamlaka ya kuidhunisha bei hizo, kila diwani alieleza changamoto anazozikabili katika sekta yake na hata kuuliza maswali, kuchangia mawazo na tathmini tofauti kwa lengo la kuimarisha maendele ya sekta hiyo.
OY_3_8c84a.jpg
Pichani ni viongozi hao wa IRUWASA wakipata chakula, kutoka kushoto ni Mkurugenzi mtendaji wa IRUWASA, Bw. Martin Mfugale, katikati ni mgeni rasmi katika semina hiyo ambaye pia ni mwenyekiti wa bodi ya IRUWASA, Bw. Muhongole na meya wa IRUWASA, manispaa ya Iringa.
Katika semina hiyo, Madiwani hao walijadili masuala mengine kama vile bei za maji, utozaji wa bei za maji, upangaji wa bei pia malengo ya bei zinazopangwa na IRUWASA.
Mkurugenzi mtendaji wa IRUWASA, Bw. Martin Mfugale alikuwa akijibu maswali ya madiwani hao ambao walitaka kujua kuhusu msimamo wa mamlaka hiyo katika changamoto zinazotokea, na jinsi watakavyozikabili ili kuinua na kuimarisha sekta hiyo katika manispaa ya Iringa.
Mamlaka hiyo ilitoa zawani nono kwa baadhi ya wahudumu wake ambao ni watuamiaji na walipaji bili bora, washindi walitunukiwa vyeti vya heshimu na kiasi kadhaa cha fedha kwa kila mmoja kama motisha kutokana na mchango wao unaopelekea maendeleo ya mamlaka hiyo pia jamii inayowazunguka, hivyo IRUWASA ina dhamiria kuboresha suala la UHAKIKA WA MAJI NA NISHATI, kauli mbiu inayoenda sambamba na kaulimbiu ya kimataifa (Dunia) ambayo ni WATER AND ENERGY inayotumika kote ulimwenguni.
OY_4_57923.jpg
baadhi ya madiwani wakiwa katika foleni tayari kwa kuchukua chakula
OY_2_0e398.jpg
Mmoja kati ya washindi waliozawadiwa katika semina hiyo, Bw. Samweli Kinyunyu akipokea bahasha ya fedha.
12_a5554.jpg
Watumishi wa IRUWASA walipopata picha ya pamoja baada ya kusisha zoezi hilo jana.
Share:

200 WAUAWA VIJIJINI NIGERIA

NIG_351d1.jpg
Watu wa kabila la Fulani katika kijiji kilioko kwenye kiunga cha mji mkuu wa Nigeria Abuja.
Takribani watu 200 wameuwawa na watu wenye silaha katika mashambulizi yaliofanyika kwenye vijiji vitatu katikati ya Nigeria. Mashambulizo ya Jumamosi yamefuatiwa na ya jana katika jimbo la kaskazini mashariki la Taraba.
Mauaji hayo yanayotokana na mizozo ya malisho, n'gombe na dini yanayoendelea kupamba moto nchini Nigeria.
Katika kadhia zote mbili wafugaji wa kabila la Fulani wanashukiwa kuhusika na mashambulio hayo.Msemaji wa polisi amethibitisha kutokea kwa mashambulizi hayo vijijini lakini hakutowa idadi ya maafa. Idadi ya watu 200 waliouwawa imezingatia makadirio ya idadi ya wahanga katika kila kijiji. Imeripotiwa kwamba washambuliaji kadhaa wakiwa na silaha nzito waliingia katika vijiji vya Ungwar Sankwai, Ungwar Gala na Chenshyi hapo Jumamosi.Mkaazi mmoja wa kijiji cha Chenshyi Nuhu Moses amekaririwa na kituo cha habari cha Nigeria CKN akisema nyumba zote zimeteketezwa na watu waliojaribu kukimbia waliuwawa kwa kupigwa risasi. Wahanga ni pamoja na mchungaji na wanawe.

Chifu mmoja wa jadi ambaye amekataa kutaja jina lake kwa kuhofia kushambuliwa amesema wanaume na wanawake, watoto na wazee waliuwawa kwa kupigwa risasi na kukatwa kwa mapanga wakati wengine waliteketezwa na moto majumbani mwao.
Chifu huyo amewaambia waandishi wa shirika la habari la Sahara kwamba pia watu wao wengi wamechukuliwa misituni na washambuliaji hao kutoka vijiji vyote.
Wahusika kusakwa.
Gavana wa jimbo la Kaduna Mukhtar Ramalan Yero ameapa kuwafikisha mbele ya mkono wa sheria wahusika wa mauaji hayo na ameamuru kufanyika kwa uchunguzi kamili na polisi tayari wametumwa kwenye vijiji vilivyoathirika na mashambilizi hayo.
Kaduna Kusini imekuwa ikishuhudia mashambulizi ya mara kwa mara yanayofanywa na wafugaji wa kabila la Fulani tokea kuzuka kwa ghasia za baada ya uchaguzi wa mkuu wa mwaka 2011.
Shambulio la Jumamosi limekuja katika kipindi kisichozidi saa 24 baada ya shambulio kama hilo katika jimbo la Benue ambapo washambuliaji wanaotuhumiwa kuwa wa kabila la Fulani walivamia vijiji kadhaa na kuuwa watu zaidi ya 30.
Mauaji yanaendelea.
Mapema wiki hii washambuliaji wanaoaminika kuwa wezi wa n'gombe wa kabila la Fulani waliuwa takribani watu 133 katika vijiji kadhaa kwenye jimbo la Katsina.
Mamia ya watu wameuwawa mwaka jana katika mapambano kati ya wachunga n'gombe wa kabila la Fulani ambao wengi wao ni Waislamu na jamii za Wakristo kama vile za kabila la Berom katika eneo tete la Nigeria ya kati ambapo ndipo sehemu kubwa ya Wakristo wa kusini inapokutana na Waislamu wa kaskazinii.
Machafuko ya Nigeria ya kati kwa kawaida hayahusiani na uasi wa kundi la Boko Haram huko kaskazini mashariki ya Nigeria lakini wachambuzi wanahofia kundi hilo lenye mafungamano na kundi la Al Qaeda linalotaka kutumika kwa sheria kali za Kiislamu kaskazini mwa Nigeria linaweza kuutumia mzozo wa Nigeria ya kati kwa faida yao.
Chanzo, dw.de/Swahili
Share:

WATU WATATU WAKAMATWA HUKO MOMBASA

Polisi mjini Mombasa wamemkamata mshukiwa wa tatu wa ugaidi na kunasa silaha zaidi katika gari lililokuwa limebeba mabomu mawili Jumatatu jioni katika mtaa wa Changamwe.
Mshukiwa huyo alikamatwa na polisi wa kupambana na ugaidi waliopata taarifa kutoka katika idara ya ujasusi na mashirika mengine ya usalama.
Inaaminika kuwa mshukiwa huyo alikuwa kiongozi wa njama ya shambulizi iliyotibuka na alikuwa ametoroka wakati washukiwa wenzake wawili walipokamatwa Jumatatu jioni.
Washukiwa waliokamatwa Jumatatu walikuwa wanapanga kufanya mashambulizi katika sehemu ambazo hawakutaja mjini Mombasa.
Walitarajiwa kufikishwa mahakamani Jumanne ingawa polisi waliomba muda zaidi kufanya uchunguzi.
Kwa mujibu wa kamishna mkuu wa Mombasa, wataalamu wa mabomu walitegua mabomu hayo.
Pia walinasa mitungi sita yenye uzito wa kilo 60 yenye uwezo wa kulipua majengo, maguruneti sita, bunduki aina ya AK-47 na risasi 270 pamoja na vifaa vitano vya kulipua mabomu ikiwemo simu ya mkononi.
Maafisa wa ujasusi waliweza kunasa mawasiliano yao na kuweza kuwakamata washukiwa hao.
Mombasa ni mji unaosifika kwa utalii lakini hivi karibuni umekuwa ukikumbwa na harakati za vijana wa kiisilamu kukumbatia itikadi kali za kidin
Share:

IRINGA MJINI LEO

IMG_0005_e2038.jpg
taswira halisi ya Manispaa ya Iringa leo mchana.
Picha na JAYRICK
Share:

Wito watolewa kwa Israel na Palestina


obama_07306.jpg
Rais Mahmoud Abbas akiwa na Rais Barack Obama.
Rais wa Marekani Barack Obama amemshinikiza Kiongozi wa Mamlaka ya Palestina, Mahmoud Abbas, kusaidia kuondoa mkwamo katika mazungumzo ya amani kati yake na Israel.
Aidha, Rais Obama amewataka viongozi wa nchi hizo mbili kufanya maamuzi magumu ya kisiasa ili mazungumzo hayo yaweze kusonga mbele.
Akizungumza na Abbas katika Ikulu ya Marekani, Rais Obama amezitaka Palestina na Israel kukubaliana kuhusu mfumo wa kuendelea na mazungumzo ya amani ya Mashariki ya Kati yanayosimamiwa na Marekani, ambayo muda wake utakamilika Aprili 29, mwaka huu.
Abbas ambaye amekwenda nchini Marekani wiki mbili baada ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ameonya kuwa muda unapita huku mazungumzo hayo yakisuasua na kuitaka Israel kuwaachia huru wafungwa wa Palestina ifikapo mwishoni mwa mwezi huu wa Machi, ili kuonyesha kuwa wako tayari na makini kwa juhudi za amani ya Mashariki ya Kati.

Abbas alikaa pembeni ya Rais Obama, katika kiti kilichokaliwa wiki mbili zilizopita na Netanyahu, ambaye alilalamika kuwa Israel imetekeleza mipango yake kama sehemu ya mazungumzo hayo ya amani, huku Palestina ikiwa haijatekeleza kwa upande wake.
Rais Obama amesema kuwa makubaliano hayo yanapaswa kuzingatia misingi ya mipaka ya taifa la Palestina iliyowekwa miaka 47 iliyopita.
Abbas apuuzia madai ya Israel.
Akipuuza madai ya Israel kutaka itambuliwe kuwa taifa la Wayahudi, Abbas alimkumbusha Rais Obama kuwa Wapalestina wamekubali uhalali wa Israel tangu mwaka 1988 na kwamba mwaka 1993 walilitambua taifa la Israel.
Baada ya kukutana na Rais Obama, Abbas pia alikuwa na mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry, ambapo pamoja na mambo mengine walibadilishana mawazo kuhusu uwezekano wa kusonga mbele mazungumzo hayo.
Kwa upande mwingine mpatanishi Mkuu wa Palestina katika mazungumzo ya amani ya Mashariki ya Kati, Saeb Erekat, amesema Israel lazima ichague kati ya kujenga makaazi ya Walowezi katika Ukingo wa Magharibi na makubaliano ya amani, lakini haiwezi kufanya mambo yote hayo mawili.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Jumatatu, Erekat amesema kuwa makubaliano yoyote lazima yahusishe eneo la mipaka lililochorwa la taifa la Palestina, lililowekwa mwaka 1967, kabla Israel haijalitwaa kimabavu eneo la Ukingo wa Magharibi, Gaza na Jerusalem Mashariki.
Chanzo dw.de/SwahilI
Share:

CHELSEA HIYOOO..... ROBO FINALI LIGI YA MABINGWA ULAYA


Samuel Eto'o akishangilia baada ya kuifungia Chelsea bao la kwanza dakika ya nne Uwanja wa Stamford Bridge

Prolific: The goal was the African forward's 30th strike in the Champions League
Hilo lilikuwa bao la 30 la Mwafrika huyo tishio kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya
Cushion: Cahill's strike extended Chelsea's aggregate lead to 3-1 and sent them towards the last eight
Cahill akiifungia Chelsea na kukamilisha ushindi wa jumla wa 3-1 kwa michezo yote miwili ilichezwa
Jumping for joy: Chelsea players celebrate Cahill's goal on the stroke of half-time
Wachezaji wa Chelsea wakisherehekea ushindiReturn: Former Chelsea striker Didier Drogba emerges from the tunnel for Galatasaray
Mshambuliaji wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba akiingia Uwanja wa Stamford Bridge na timu yake ya Galatasaray
Reunited: Drogba hugs Chelsea manager Jose Mourinho before the game
 Drogba akikumbatiana na kocha wa Chelsea, Jose Mourinho kabla ya mechi
Hero: A banner saluting former striker Drogba on show at Stamford Bridge during the game
Bango la kumpa heshima yake Drogba likiwa limetungikwa Stamford Bridge wakati wa mechi
CHELSEA itaendelea kupeperusha bendera ya England kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya usiku huu kuitoa Galatasaray ya Uturuki kwa jumla ya mabao 3-1 Uwanja wa Stamford Bridge, London.
Baada ya kutolewa kwa Manchester City na Arsenal katikati ya wiki iliyopita, Chelsea imejikatia tiketi ya kuingia Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa kwa kuifunga mabao 2-0 timu hiyo ya mchezaji wao wa zamani nyota, Didier Drogba.
Mabao ya Chelsea yamefungwa Samuel Eto'o 'Kikongwe' dakika ya nne na Gary Cahil dakika ya 43. Katika mchezo mwingine usiku huu, Real Madrid imeifunga Schalke mabao 3-1 Uwanja wa Santiago Bernabeu na kuwatoa Wajerumani hao kwa jumla ya mabao 9-2 baada ya awali kushinda 6-1 ugenini. Leo mabao ya Real yalifungwa na Cristiano Ronaldo dakika ya 21 na 74 na lingine Alvaro Morata dakika ya 75, wakati la Schalke limefungwa na Tim Hoogland dakika ya 31
Share:

MAGAZETI YA LEO



DSC 0140 8a85f
DSC 0141 feb1a
DSC 0142 9d068
DSC 0143 c7a89
DSC 0144 25fdd
DSC 0145 6fc17
DSC 0146 9f7e1
DSC 0147 4f780
DSC 0148 7bb62
DSC 0149 474b5
DSC 0150 c7e49
DSC 0151 e501f
DSC 0152 714f6
DSC 0153 b1a83
DSC 0154 b6c60


Share:

WARIOBA AFUNGUKA

maggid_d626c.jpg
Warioba na kukata ngebe wapi na wapi ? Hapa hakuna Simba kukata ngebe za Yanga na kinyume chake. Katiba ya ni jambo muhimu sana kwa mustakabali wa nchi. Tukemee uwepo wa ushabiki wa vyama na yote yenye kufanana na ushabiki wa Simba na Yanga...
Maggid,Dar es salaam
Share:

KILA KIJIJI NDANI YA JIMBO LA CHALINZE KUPATA TREKTA KWA AJILI YA KILIMO - RIDHIWANI KIKWETE

Displaying TALAWANDA 1 (5).jpg
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM,Ridhiwani Jakaya Kikwete  akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Mindukene,Kata ya Talawanda ndani ya Jimbo la Chalinze leo Machi 18,2014.Katika Mikutano yake kwenye Vijiji vya Mindukene, Msigi na Kisanga ndani ya Jimbo hilo,Ridhiwani Kikwete ameahidi kuhakikisha vijiji vyote kwenye jimbo hilo vinakuwa na matrekta ili kuboresha kilimo.Picha na Othman Michuzi
k_d6354.png
- Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM,Ridhiwani Jakaya Kikwete akifurahia jambo na Mzee Joseph January wa Kijiji cha Kisanda,Kata ya Talawanda ndani ya Jimbo la Chalinze.Picha na Othman Michuzi
Displaying TALAWANDA 1 (6).jpg
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM,Ridhiwani Jakaya Kikwete  akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Msigi,Kata ya Talawanda ndani ya Jimbo la Chalinze leo Machi 18,2014.Picha na Othman Michuzi
MGOMBEA wa Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani, Ridhiwani Kikwete ameahidi kuhakikisha vijiji vyote kwenye jimbo hilo vinakuwa na matrekta ili kuboresha kilimo kiwe na tija.
Alitoa ahadi hiyo wakati wa mikutano ya kampeni kwenye vijiji vya Mindukene, Msigi, Kisanga vyote vikiwa kwenye kata ya Talawanda.
Kikwete alisema kuwa wakulima wengi bado wanatumia jembe la mkono ambalo haliwezi kuwaletea manufaa wala kuboresha kilimo ambacho ni tegemeo lao.
"Nikianikiwa kupata ubunge nitahakikisha kila kijiji kinakuwa na matrekta kwa ajili ya kuwa na wakulima ambao wataweza kulima kwa faida kwa ajili ya chakula na ziada kuuza ili kujiongezea kipato," alisema Kikwete.
Akizungumzia changamoto ya migogoro ya wakulima na wafugaji alisema kuwa atahakikisha anazikutanisha pande zote ili kujua chanzo cha migogoro hiyo.
"Tatizo kubwa ni viongozi kushindwa kuzikutanisha pande zinazohusika badala yake wanaongea na upande mmoja jambo ambalo haliwezi kumaliza migogoro hiyo ambapo njia pekee ni kuwa na matumizi bora ya ardhi kwa kutenga maeneo kwa wakulima na wafugaji," alisema Kikwete.
Aidha alisema kuwa migogoro hiyo inatokana na wafugaji kuingia kinyemela pasipo kufuata taratibu bila ya kupitia kwenye mikutano mikuu ya serikali za vijiji.
Katika hatua nyingine aliwataka wazazi kuepukana na tabia ya kuuza kiholela maeneo yao hali ambayo itasababisha vijana kukosa ardhi kwa ajili ya kilimo na makazi.
Aliongeza kuwa atahakikisha anaboresha masuala mbalimbali ikiwemo sekta ya elimu, afya, miundombinu, kilimo, mikopo kwa vijana na akinamama, uzinduzi rasmi wa kampeni unatarajiwa kufanyika kesho Aprili huko Chalinze na uchaguzi utafanyika Aprili 6 mwaka huu.
Share:

WARIOBA AWAKUNA WASOMI


Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Profesa Palamagamba Kabudi (kushoto) akizungumza na Mjumbe mwenzake, Prof Costa Mahalu katika Viwanja vya Bunge hilo, mjini Dodoma jana. Picha na Michael Jamson
Baadhi ya wasomi na wachambuzi wa masuala ya kisiasa hapa nchini wamesema hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Mabadilko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba itasaidia kubadilisha msimamo wa wajumbe wengi wa Bunge Maalumu la Katiba.
Kauli hiyo imekuja muda mfupi baada ya Jaji Warioba kuwasilisha Rasimu ya Pili ya Katiba katika Bunge hilo tayari kwa kuijadili, kuiboresha na hatimaye kutoka na Rasimu ya Tatu itakayopigiwa kura ya ama kuikubali kuwa Katiba Mpya au la.
Mwanasiasa mkongwe, Njelu Kasaka alisema hotuba hiyo imesaidia kutoa uelewa wa mambo kwa kuwa idadi kubwa ya wajumbe ndani ya Bunge hilo hawakuwa na uelewa juu ya hoja mbalimbali zilizopendekezwa kwenye rasimu hiyo.
"Kutokana na ufafanuzi huo, wengi watakuwa wameelewa kwa nini Tume iliamua kupendekeza muundo wa Serikali Tatu na wala siyo mbili. Itasaidia pia kuwajengea uwezo wa kuhoji katika mijadala ya Kamati itakapoanza kukaa rasmi," alisema Kasaka ambaye alikuwa miongoni mwa Wabunge 55 walioasisi Kundi la G55 lililotaka kuundwa Serikali ya Tanganyika mwaka 1993.
"Lakini jambo jingine hotuba hii imeondoa ni unafiki na imewaaibisha kwa unafiki wao baadhi ya watu, kwa sababu pamoja na kuongoza Serikali moja ya Jamhuri ya Muungano, imefahamika wazi kwamba Waziri Mkuu kumbe hana mamlaka yoyote yale katika upande wa Zanzibar."
Kwa upande wake, Profesa Boniventure Rutinwa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), aliunga mkono hoja hiyo akisema kinachotakiwa kwa wajumbe hao ni kujenga imani, kuondoa tofauti zao na kutokubaliana na hoja zenye masilahi ya vyama na makundi yao badala ya Taifa.
"Kinachotakiwa kwa sasa ni kupima uwezekano kwa kuhoji, je, pamoja na ufafanuzi huo, Serikali Tatu inaweza kuwa mwarobaini wa kumaliza changamoto zote? Lakini pia wanatakiwa kufahamu kwamba inawezekana kuna changamoto nyingine ambazo zinaweza kujitokeza katika muundo huo," alisema Profesa Rutinwa.
Kwa upande wake, Profesa Penina Mlama aliwataka wajumbe wa Bunge hilo kuchukua hoja hizo na kufikiri kwa mapana zaidi wakati wa majadiliano ili kuondoa athari zinazoweza kujitokeza baadaye.
"Wamerahisishiwa, na kazi imebakia kwao kupima na kufikiria zaidi hotuba hii. Wajumbe watambue kwamba si mawazo ya Jaji Warioba yaliyowasilishwa pale, bali ni mawazo ya Watanzania, ambayo yanatakiwa kupokewa kwa mtazamo chanya ili wasije kuaibika baadaye iwapo watashindwa kufanya uamuzi sahihi," alisema.
Mjumbe wa Bunge, James Mapalala alisema Jaji Warioba amemaliza kazi ya kuelimisha juu ya umuhimu wa Serikali Tatu na anaamini watakaosimama kumpinga wataona haya
Share:

Jumapili, 16 Machi 2014

KINAENDA KUPIGWA CHA ARSENAL

Share:

FIRST 11 YA LEO

Chukwuemeka Aneke     Chukwuemeka Aneke     2010/11     2013/14     Not Active
Mikel Arteta     Mikel Arteta     2004/05     2013/14     Active
Héctor Bellerín     Héctor Bellerín     2012/13     2013/14     Active
Nicklas Bendtner     Nicklas Bendtner     2004/05     2013/14     Active
Santiago Cazorla     Santiago Cazorla     2012/13     2013/14     Active
Marouane Chamakh     Marouane Chamakh     2009/10     2013/14     Active
Vassiriki Abou Diaby     Vassiriki Abou Diaby     2005/06     2013/14     Active
Johan Djourou     Johan Djourou     2004/05     2013/14     Not Active
Thomas Eisfeld     Thomas Eisfeld     2011/12     2013/14     Not Active
Lukasz Fabianski     Lukasz Fabianski     2006/07     2013/14     Active
Mathieu Flamini     Mathieu Flamini     2003/04     2013/14     Active
Emmanuel Frimpong     Emmanuel Frimpong     2008/09     2013/14     Active
Gervinho     Gervinho     2010/11     2013/14     Active
Kieran Gibbs     Kieran Gibbs     2005/06     2013/14     Not Active
Olivier Giroud     Olivier Giroud     2011/12     2013/14     Active
Serge Gnabry     Serge Gnabry     2012/13     2013/14     Not Active
Isaac Hayden     Isaac Hayden     2013/14     2013/14     Active
Alex Iwobi     Alex Iwobi     2013/14     2013/14     Active
Carl Jenkinson     Carl Jenkinson     2010/11     2013/14     Not Active
Laurent Koscielny     Laurent Koscielny     2009/10     2013/14     Active
Share:

HIYO NDO FIRST 11 YA ILIYO CHEZA LEO

Player
First Season Last Season Status
Ben Amos Ben Amos 2007/08 2013/14 Not Active
Alexander Büttner Alexander Büttner 2012/13 2013/14 Not Active
Michael Carrick Michael Carrick 1998/99 2013/14 Active
Tom Cleverley Tom Cleverley 2006/07 2013/14 Not Active
Jonny Evans Jonny Evans 2005/06 2013/14 Not Active
Patrice Evra Patrice Evra 2005/06 2013/14 Active
Fabio Fabio 2007/08 2013/14 Active
Marouane Fellaini Marouane Fellaini 2008/09 2013/14 Active
Rio Ferdinand Rio Ferdinand 1995/96 2013/14 Not Active
Darren Fletcher Darren Fletcher 1999/00 2013/14 Not Active
David de Gea David de Gea 2010/11 2013/14 Active
Ryan Giggs Ryan Giggs 1992/93 2013/14 Active
Angelo Henriquez Angelo Henriquez 2012/13 2013/14 Not Active
Javier Hernández Javier Hernández 2009/10 2013/14 Active
Adnan Januzaj Adnan Januzaj 2012/13 2013/14 Active
Phil Jones Phil Jones 2009/10 2013/14 Active
Shinji Kagawa Shinji Kagawa 2011/12 2013/14 Active
Michael Keane Michael Keane 2010/11 2013/14 Not Active
Anders Lindegaard Anders Lindegaard 2010/11 2013/14 Active
Jesse Lingard Jesse Lingard 2010/11 2013/14
Share:

MATUKIO YA VIDEO

Kumbukumbu la Blogu

Recent Posts

Unordered List

Pages

Theme Support

Sample Text