Wasanii wazindua kampeni ya kitaifa kuishinikiza serikali kuwatambua katika katiba
Leo asubuhi (February 28) pande za Kinondoni Vijana Social Hall kulikua wasanii wa fani mbalimbali waliokuwa wamekusanyika kwa ajili ya kuzindua kampeni ya kitaifa maalum kwa ajili ya kuishinikiza serikali kuwatambua wasanii kikatiba.
Licha
ya kuwa na shinikizo hilo lakini pia kutakuwa na maandamano ya amani
wanayotarajia kuyafanya ikiwa ni sambamba na kumpongeza Rais Jakaya
Kikwete kwa kumteua mmoja wao (hajafahamika bado) washiriki kuhudhuria
katika bunge la katiba.
tumepiga na nikki wa pili moja kati wasanii waliopo
mstari wa mbele kwenye movement hii
Nikki pia amezungumzia azimio wanalotaka kuliweka
"Tunataka kufanya azimio la kuhakikisha kuwa eidha siku moja au wiki nzima kazi yoyote ya sanaa isiskike kwenye media, Radio Tv magazeti, naposema sanaa kuanzia mziki, katuni, graphics chochote, na kama ni mziki hata mziki wa nje usipigwe maana sisi hapa ni mabalozi wa wasanii wengine duniani, ili watu watambue mchango wa wasanii na watusikilize"
"Tumezindua
kampeni yetu ya kitaifa kushinikiza serikali itambue wasanii kama kundi
maalum kwenye jamii na kuingizwa kwa haki bunifu katika katiba hizo
ndio hoja zetu mbili tunazozipigia kelele" amesema Nikki wa Pili
lakini
pia ameendelea kusema "Tutafanya maandamano na kumfahamisha Raisi
Jakaya Kikwete kuwa sekta ya ubunifu inaingiza mapato kuliko sekta ya
Nishati na Madini ambayo inajadiliwa kila siku bungeni, lakini sekta ya
ubunifu imesahaulika"
Nikki pia amezungumzia azimio wanalotaka kuliweka
"Tunataka kufanya azimio la kuhakikisha kuwa eidha siku moja au wiki nzima kazi yoyote ya sanaa isiskike kwenye media, Radio Tv magazeti, naposema sanaa kuanzia mziki, katuni, graphics chochote, na kama ni mziki hata mziki wa nje usipigwe maana sisi hapa ni mabalozi wa wasanii wengine duniani, ili watu watambue mchango wa wasanii na watusikilize"
0 maoni:
Chapisha Maoni