• This is default featured slide 1 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

  • This is default featured slide 2 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

  • This is default featured slide 3 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

  • This is default featured slide 4 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

  • This is default featured slide 5 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

Jumamosi, 24 Mei 2014

MALARIA SASA YAFIKIA TAMATI YA KUPATA KINGA

Mbu anaesababisha malaria
Viini vya malaria
Watafiti wa Marekani wamebaini miili ya watoto hao hutoa viini vya kinga ambavyo hushambulia wadudu wanaosababisha Malaria.
Kwa kumdunga mtu sindano yenye viini hivyo vyo mtu anaweza kukingwa na ugonjwa huo .
Watafiti hao ambao walichapisha matokeo yao kwenye jarida la kisayansi , wanasema majaribio ya utafiti huo katika binadamu na katika sokwe sasa yanahitaji kutathminiwa kikamilifu ili kupata matumaini halisi ya chanjo ya malaria.(MM)
Prof Jake Kurtis, mkurugenzi wa kituo cha utafiti wa afya wa kimataifa katika hospitali ya kisiwa cha Rhode katika chuo kikuu cha tiba cha Brown , alisema : "Nadhani kuna ushahidi wa kuaminika kwamba hii inaashiria upattikanaji wa chanjo ''
" Hata hivyo wadudu wa malaria ni vigumu kuwashambulia'' . Kwa kweli ni maadui wakubwa ." aliongeza Kurtis. Utafiti huo ulianza kwa kundi la watoto wa shule 1000 nchini Tanzania , ambao sampuli za damu yao zilichunguzwa mara kwa mara katika miaka ya mwanzo ya maisha yao .
Asilimia 6 ya watoto ya watoto hawa waliweza kuwa na kinga asilia kwa malaria, licha ya kuishi katika eneo ambako ugonjwa huo umekithiri.
Share:

MUHIMU


s2_e5bc0.jpg

Uzinduzi wa chapisho la Tatu la Taarifa za Msingi za Kidemografia, Kijamii na kiuchumi linalotokana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 (Basic Demographic and Socio-Economic Profile) katika ngazi ya Taifa uliokuwa umepangwa kufanyika siku ya Ijumapili tarehe 25 Mei, 2014 umeahirishwa.
 
Uzinduzi huo sasa utafanyika rasmi tarehe 10 Juni, 2014 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwl. Julius Nyerere uliopo mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es Salaam kuanzia saa 3:00 asubuhi.
 
Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mgeni rasmi katika uzinduzi huo  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Aidha, uzinduzi huo unatarajiwa kuhudhuriwa na watu wapatao mia tano (500) ambao ni pamoja na Viongozi mbalimbali wa ngazi za juu Serikalini, Mabalozi, Wadau wa Maendeleo, Viongozi wa Dini, Viongozi wa Vyama vya Siasa, Wawakilishi wa Mashirika yasiyo ya Serikali na Wadau wa Takwimu nchini.
 
Kwa kifupi chapisho hili linatoa viashiria mbalimbali ambavyo ni pamoja na Kiwango cha uzazi, umri wa kuishi wa mtanzania, vifo vya watoto wachanga, kiwango cha vifo vya wakina mama vitokanavyo na uzazi na taarifa nyingine kwa ajili ya kupanga mipango ya maendeleo.
 
Chapisho hili ni mwendelezo wa machapisho mbalimbali yanayotolewa na Ofisi zetu mbili yaani Ofisi ya Taifa ya Takwimu na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Zanzibar kama ilivyoainishwa kwenye kalenda ya machapisho ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012.
Share:

CCM MAENDELEO DAIMA KINANA AZIDI KUCHAPA KAZI SINGIDA


1._Katibu_Mkuu_wa_CCM_Abdulrahman_Kinana_akihutubia_wananchi_kwenye_Uwanja_wa_shule_ya_sekondari_Sebuka__wilaya_ya_Ikungi_mkoani_Singida_Mei_22_2014_57131.jpg
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi kwenye Uwanja wa shule ya sekondari Sebuka,  wilaya ya Ikungi mkoani Singida, leo, Mei 22, 2014
3._Jengo_hili_lililoko_Kijiji_cha_Msimi_Kata_ya_Sepuka_wilayani_Ikungi_lilifunguliwa_na_Rais_Jakaya_Kikwete_wakati_huo_akiwa_Waziri_wa_Mambo_ya_Nje_na_Ushirikiano_wa_Kimataifa_f77b0.jpg
Jengo hili lililoko Kijiji cha Msimi, Kata ya Sepuka wilayani Ikungi, lilifunguliwa na Rais Jakaya Kikwete wakati huo akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
7._Baadhi_ya_wanachama_wapya_wa_CCM_wakila_kiapo_baada_ya_kupewa_kadi_na_Kinana_baada_ya_uzinduzi_wa_Ofisi_ya_CCM_kata_ya_Inghombwe_wilayani_Ikungi_a1b7d.jpg
Baadhi ya wanachama wapya wa CCM wakila kiapo baada ya kupewa kadi na Kinana baada ya uzinduzi wa Ofisi ya CCM kata ya Inghombwe wilayani Ikungi
Share:

Wimbo wa Pharrell 'Happy' wazua zogo Iran

140521090010_iran_happiness_video_512x288_getty_nocredit_d1b18.jpg
140521091230_iran_happiness_video_512x288_bbc_nocredit_767e0.jpg
140521092657_happy_512x288_bbc_nocredit_313f2.jpg

Kikundi cha mashabiki wa muziki nchini Iran walioiga wimbo maarufu wa mwanamuziki maarufu wa Marekani Pharrell Williams, 'Happy' wamejipata matatni baada ya kukamatwa na polisi.

Kanda ya video waliyoirekodi wakiiga wimbo huo, inaonyesha vijana watatu na wanawake kadhaa ambao hawakuwa wamejitanda mitandoa, wakicheza densi kwenye barabara za nchi hiyo na kwenye paa za nyumba mjini Tehran.
Mkuu wa Polisi, Hossein Sajedinia, alisema kuwa kanda ya video inayoonyesha vijana hao wakicheza, imekiuka maadili ya jamii.

Kituo cha televisheni ya serikali kilionyesha vijana hao wakikiri makosa siku ya Jumanne.

Inaarifiwa maelfu ya wananchi wa Iran wamekamatwa katika miaka 35 iliyopita wakisherehekea na kujiburudisha kwa mambo ambayo serikali inaona kama ya kukiuka maadili.

Hata hivyo vijana hao wanaosema ni waigizaji wanadai kuwa walihadaiwa kushiriki katika kanda hiyo na watu waliokuwa wanatafuta waigizaji wakisema ulikuwa kama mtuhani kwao.

"waliniambia kuwa wanatengeza filamu na kuwa walikuwa na kibali na ndio maana nikakubali kushiriki,'' alisema mmoja wa vijana waliokamatwa.

Mtuhumiwa mwingine alisema walionasa kanda hiyo waliwaahidi kwamba hawataisambaza.
'Wamekiuka maadili'

Kulingana na taarifa ambazo bado hazijathibitishwa, watu 13 walikamatwa kuhusiana na kanda hiyo, ingawa idadi kamili ya waliokamatwa haijatangazwa rasmi.

Pharrel aliyeteuliwa kwa tuzo la Oscar kwa wimbo wake huo mwaka huu ambao umekuwa maaruufu sana duniani, alielezea kukasirishwa na hatua ya vijana hao kukamatwa.

"yani siamini kama watoto hawa walikamatwa kwa kujaribu kueneza furaha,'' alisema Pharrell katika ukurasa wake wa Facebook.
Chini ya sheria za kiisilamu, sharti mwanamke ajitande kutoka kichwani hadi katika viganja vya mguu.

Polisi ambao jukumu lao ni kuhakikisha kuwa sheria ya mavazi inafuatwa, hushika doria mara kwa mara katika barabara za mji mkuu Tehran.

Kanda hiyo ya "Happy we are from Tehran" ilionekana kwenye mtandao wa Youtube tarehe 19 Mei na kufikia sasa imetazamwa mara 40,000.

Baadhi wametuma ujumbe wa kukejeli serikali ya Iran wakisema kuwa Iran ni nchi ambako ni hatia kwa mtu kuwa na furaha.
Wimbo halisi wa Pharrell 'Happy' umepelekea maelfu ya watu kote duniani kuiga video ya wimbo huo na kutengeza video zao wenyewe. Kutoka Kenya, Marekani , Uingereza yaani nchi nyingi duniani tu, watu wameiga video hiyo kwa kutengeza yao wenyewe.CHANZO BBC,(A,I)
Share:

Jumapili, 11 Mei 2014

MAN CITY WAIBUKA KIDEDEA

http://www.ibn-tv.com/wp-content/uploads/2014/03/Man-City.jpg
Manchester City waifunga West Ham goli 2-0 katika mechi iliyokwisha muda mfupi uliopita. Mashabiki wavamia uwanja kwa furaha ya ubingwa. Matokeo mengine: Liver 2-1 New Castle,Card 1-2 Chelsea, Hull 0-2, Everton South 1-1 Man Utd, Tot 3-0 Villa, Norw 0-2 Arsenal, Fulh 2-2 Crystal, Sunder 1-3 Swan, WBM 1-2 Stoke. (FS)
Share:

Jumatano, 7 Mei 2014

Majibu ya Nash Mc juu ya kudai kutelekeza msichana wake ambaye inasemekana ni Mjamzito.

You-heard218Huu ni muendelezo wa You heard ambayo ilianza jana alisikika msichana ambaye inasemekana alitelekezwa na Nash Mc baada ya kupata ujauzito,simulizi hiyo inaendelea na hapa pia utamsikiliza Nash Mc akiongelea kuhusu madai ya msichana huyo.
88.5 Clouds Fm inasikika ukiwa Pwani.
Share:

Kauli ya Sauti Soul baada ya kupata taarifa ya kufungiwa kwa video yao.

TZA SAUTI SOL


Ikiwa inakaribia wiki ya pili sasa tangu kundi la Sauti Soul kuachia video ambayo imeleta utata na baadae kutoka taarifa za kufungiwa,hatimae leo kuna kauli kutoka kwao kama Sauti Soul kuhusu hii video.
Miongoni mwa maoni ya watu kuhusu video hiyo ambayo bado imezua utata na hisia tofauti ni ile hali ya kuonyesha misuli iliyotajwa na mafans wa kike kama jambo la kufurahisha huku upande wa kiume wakisema kama inawadharirisha.
TZA SAUTI SOL2Kwa mujibu wa bendi nzima la Sauti Soul video ya Nishike ilitungwa tu kwa ajili ya kutuma ujumbe>>’Tuna pitisha ujumbe kwamba wanaume sharti wafanye mazoezi sio tu kupata sixpacks lakini kwa ajali ya afya yao’
‘Wengi wetu wamekua wanene kupita kiwango na njia ya pekee ya kupunguza unene huo nikupitia kufanya mazoezi kwenye gyme’.asema Delvin Mudig ambaye ni miongoni mwa waimbaji wanaounda Sauti Soul
Katika kauli nyingine Austin Chimano ambaye pia ni member wa Sauti Soul amesema>>’Hatukukiandaa video ya Nishike kukera mtu yeyote tunacheza na kuimba Kisauti Soul.tumekua sisi tu.hatukupanga kua na wimbo ulitakaozua hisia kama hizi Ilikua tu ni dhihirisho la penzi.hakukua na fumbo hapo’.
Naye Bien Aime Baraza ameongezea>>’kama bendi Sauti Soul sasa inawekwa kwenye kiwango sawa na bendi za hadhi ya juu kama P-Square, Mafikizolo,Mikasa na wengine tumekuwa kutoka wakati wa Lazizi na tungependa mafans wetu waendelee kutusapot kutuwezesha kuwa na kujulikana nje ya Bara la afrika’
Mwingine ni Polycarp Otieno ambaye yeye amesema>>’Sanaa inahusu kujieleza na kwetu haikua tu tutoe wimbo ambao watu wangeu skiza na kuridhika,lakini kitu ambacho kiingeonyesha hilo kwenye video,ndio tumepata maoni mabaya kutoka kwa wanaume,lakini tunawajibu kua ‘usimchukie mchezaji’, kwa kweli video inayotokea niya kuwahamazisha watu wafanye zoezi’.
Share:

UJIO MPYA NIKI WA PILI

Nikki wa II - Staki KaziMshindi wa tuzo ya wimbo bora wa Hip hop Nikki wa pili leo ametoa cover ambayo inamaanisha ujio wake mwingine unaofuata baada ya Nje ya box ambayo ilitoka siku ya Valentine February 14 2013,ingawa katikati kuna single kadhaa zimetoka kwa kundi kama Weusi ambao nao ndiyo wameibuka na ushindi wa kundi bora 2013/2014.
Wimbo unaitwa Sitaki kazi haijafahamika bado kilichoimbwa ndani ni nini ila kilichoelekezwa ni tarehe rasmi ya kuachiwa kwa wimbo huo ambao itakua ni Mei 13 na imetengenezwa na producer yule yule wa Nje ya box,bei ya mkaa na baadhi ya hits za Weusi,ndani humu kawakutanisha Ben Pol na G nako
Share:

MAAJABU THIS MAN HAS NOT TAKEN A BETH SINCE 1954

hadji
Amou Hadji made headlines this week after a story circulated that he hasn’t bathed himself in 60 years. The 80-year-old Iranian man sat down for a brief photo series that details what could happen to the human body.
Not surprisingly, Hadji has a deep odor and his skin is tough and scaly. Hadji is homeless and refuses to eat food or drink clean water. His favorite food is dead porcupine and he regularly smokes a pipe filled with animal feces. Hadji claims that he has chosen this lifestyle to stay in touch with with the earth.
From the Tehran Times:
The last record of longest time going without showers belonged to a 66-year-old Indian man, Kailash Singh, who had not taken a bath over 38 years.
Not to our surprise, when we searched the reason behind Amou Haji’s way of life, we found out that he had gone through some emotional setbacks in his youth and from then on decided to live an isolated life.
He escaped from the hands of a few young men who offered him free shower, because he believes cleanliness brings him sickness.
Share:

MAREKANI YAA HIDI KUISAIDIA NIGERIA DHIDI YA WASICHANA WALIO MATEKA

obama_51ea4.jpg
Marekani imetangaza kwamba imetuma kikosi cha wataalamu nchini Nigeria kusaidia kuwatafuta wasichana takriban 200 wa shule waliotekwa nyara mwezi uliopita na wapiganaji wa kundi la Boko Haram.
Rais Barack Obama ameshutumu utekaji nyara wa wasichana hao na kusema kuwa mataifa yanapaswa kufanya kazi kwa pamoja ili kulikomesha Boko Haram.
"Tayari tumetuma kundi letu Nigeria. Wamekubali msaada wetu ambao unashirikisha wanajeshi, wadumishaji wa sheria na mashirika mengine ambao wanajaribu kutambua waliko wasichana hawa ili wawape msaada," Rais Obama alisema.
Rais Obama amesema kuwa jamii ya kimataifa inapaswa kutumia utekeji wa kikatili wa wasichana hao kama msingi wa kuungana na kuangamiza Boko Haram.
Nchini Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan amekubali msaada huo kama alivyosema msemaji wake, Daktari Reuben Abati.
"msaada huo kutoka kwa Rais Obama uliwasilishwa na Waziri wa
Share:

ZITTO AWA KIVUTIO KWENYE MAZISHI YA BABA YAKE FILIKUNJOMBE



Kutoka  kushoto mkuu wa wilaya ya  Ludewa  Juma Madah ,mbunge wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe na mbunge wa jimbo la  kigoma kaskazani Zitto Kabwe wakiwa katika msiba wa babake Filikunjombe mjini Ludewa jana.


DC Ludewa Bw Juma Madaha akitambulisha  viongozi mbali mbali







Mbunge wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe kushoto  akilitazama jeneza lenye mwili wa babake marehemu  Frolian Filikunjombe likiingizwa  ndani ya kanisa la RC Ludewa kwa ajili ya ibada ya mwisho kabla ya mazishi  yaliyofanyika katika makaburi ya Ludewa mjini



Na Francis Godwin Blog 
MBUNGE  wa  jimbo la Kigoma Kasikazin Zitto (CHADEMleo amegeuka  kuwa  kivutio  kikubwa  katika mazishi ya babake mbunge wa  jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe huku wananchi  wa  jimbo  hilo na viongozi wa CCM mkoa  wa Njombe  wakimbebesha majukumu  ya ubovu wa barabara  kwa  kumtaka  kushirikiana na mbunge wao  kuwasha moto bungeni .
Zitto  ambae  katika msafara  wake  huo  aliongozana na mbunge wa  jimbo la Mwibara Kangi  Lugola (CCM) mbunge wa  viti maalum mkoa wa  Tanga Amina Mwidau (CUF) na  wengine wa CCM nusuru avuruge  msiba  huo baada ya  wananchi  kuonyesha  kuvutiwa na uwepo  wake na  kumtaka   kusikia  sauti  yake .
Awali  wakati wa utambulisho  wa  viongozi wa kitaifa  uliofanywa na mkuu wa  wilaya ya   Ludewa Juma Madaha  waombolezaji  baada ya  kusikia  jina la Zitto Kabwe  katika orodha ya wabunge hao ndipo  sauti  ziliposikika  kuwa  wanahitaji azungumze .
Hata hivyo  katika  salam  zake katibu wa itikadi na uenezi wa CCM mkoa wa Njombe Honoratus Mgaya mbali ya  kumpongeza  mbunge Kabwe kwa  kufika katika msiba   huo na timu  yake bado  alimtaka  Kabwe na timu  yake  kusaidiana na mbunge  wao Filikunjombe kupigania ujenzi wa barabara ya lami kati ya Ludewa na Njombe.
"Mheshimiwa  Zitto Kabwe wewe ni mmoja kati ya wapiganaji wa kweli  bungeni kama  alivyo mbunge  wetu na jembe  letu wana Ludewa  Deo Filikunjombe ....sasa tunaamini mmeona ubovu wa barabara ya Njombe - Ludewa hivyo  kupitia ninyi  sisi  wana Njombe na Ludewa  tunaomba msaidiane na Filikunjombe kupigania suala la ubovu wa barabara na sio  kutoka nje ya bunge pindi suala la ubovu wa  miundo mbinu linapotolewa na mbunge  wetu"
Kufuatia  ombi hilo la Mgaya  waombolezaji walilipuka kwa  furaha   huku Zitto  Kabwe  akionyesha kuguswa na ombi hilo na kumtania mbunge wa  viti maalum mkoa wa Tanga Amina Mwidau (CUF)  kuwa UKAWA hao .
Zitto Kabwe  ambae alikuwa ni mmoja wa abiria  waliosafiri pamoja na babake Filikunjombe mzee Frolian Filikunjombe kabla ya kufariki  dunia akiwa  ndani ya ndege  kutoka  Dubai kuja nchini ni  mmoja  wa   marafiki  wakubwa wa mbunge Filikunjombe na pia ni mwenyekiti wa kamati ya PAC ambapo  Filikunjombe ni makamu mwenyekiti wake.
Hata  hivyo  alisema  kuwa  ombi la  wana Ludewa  kwake atalifanyia kazi na  kuwa suala la siasa lina  sehemu yake na yanapozungumzwa mambo ya kimaendeleo siasa  za  vyama zinawekwa kando .
Hivyo  alisema  kuwa kutokana na mahusiano mema  kati yake ya mbunge Filikunjombe ameguswa na msiba  huo na kuwa pindi atakapofika  bungeni maombi ya  wana Ludewa atayatendea kazi
Share:

Jumanne, 6 Mei 2014

Picha za jinsi mpenzi wa yule bilionea mbaguzi wa Marekani anavyokwepa waandishi

Screen Shot 2014-05-06 at 4.17.32 PMHuyu mrembo anaitwa V Stiviano ambae ndio alivujisha maongezi ya simu kati yake na bilionea Donald Sterling ambae alitoa maneno mazito yenye ubaguzi dhidi ya watu weusi kwa kusema hataki kuwaona watu hao wakihudhuria kwenye mechi za timu ya basketball anayoimiliki iitwayo L.A Clippers.
Toka hii ishu imevuja Stiviano ambae alikua ni ‘nyumba ndogo’ ya Donald amekua akikwepa waandishi wa habari ambapo aliamua kuvaa kifaa maalum kabisa ili kuepuka kuhojiwa na waandishi wa habari.
Mmoja kati ya Wamarekani waliotoa maoni yao kuhusu Stiviano alisema ‘huyu binti anaweza kuwa mpuuzi wa kupindukia… japokua mimi ni Mweusi, sijali kama Donald alikua mbaguzi ama la… msichana kama huyu anawezaje kumsaliti mtu aliempa magari ya kifahari Ferarri, Bentley mbili na nyumba ya kifahari? huyu binti hajatenda haki’
Screen Shot 2014-05-05 at 1.25.55 PM
Bilionea wa kimarekani Donald Sterling alikiri kwamba sauti iliyosikika ikitoa maneno ya kibaguzi ni yake hivyo akaadhibiwa kwa kutojihusisha na timu yake milele na kulazimishwa kuiuza timu hiyo.
Screen Shot 2014-05-05 at 1.26.24 PM
Screen Shot 2014-05-05 at 1.25.42 PM
Screen Shot 2014-05-05 at 1.25.20 PM
Screen Shot 2014-05-05 at 1.25.06 PM
Screen Shot 2014-05-05 at 1.24.40 PM
V Stiviano na Donald
V Stiviano na Donald
Share:

DAR MVUA ZA ZIDI NYESHA

20140503_062645_4cb15.jpg
20140503_062717_6a919.jpg
Hapa ni makutano ya mtaa wa Uhuru na Msimbazi Kariakoo Jijini Dar es salaam leo asubuhi.(Awadh Ibrahim wa Mjengwa blog).
Share:

JAJI BOMAN ASEMA WAANDISHI WAANDIKE HABARI ZA KUMKOMBOA MWANANCHI


DSC_0083
Mshehereshaji ambaye ni Mwanakamati ya maandilizi ya maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014, Usia Nkhoma Ledama akiwatambulisha baadhi ya waandishi wa habari wakongwe (hawapo pichani) kwa mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani.(Picha zote na Zainul Mzige). (FS)
Na Mwandishi wetu
Jaji Mstaafu Mark Bomani amesema lengo la mchakato wa Katiba ni kuhakikisha kwamba Tanzania inapata Katiba ambayo ni bora zaidi kuliko zote itakayoshughulikia changamoto na kuweka mazingira ambayo yatamrahisishia maendeleo mwananchi kwa haraka.
Akitoa risala katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani leo katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC jijini Arusha, Jaji Mstaafu Mark Bomani, amesema jukumu la mwanahabari ni kuwaelimisha baadhi ya wabunge wa Bunge Maalum la Katiba ambao hawana uelewa mkubwa na mchakato wa Katiba hawajui maana halisi ya Katiba mambo ambayo yanasababisha kujadili Katiba hiyo kwa maneno mabaya, kutishiana, matusi na kejeli.
“Zoezi la mchakato wa Katiba ni kubwa na wabunge wengi wa Bunge Maalum la Katiba hawaelewi wajibu wao katika kuijadili Katiba hiyo matokeo yake ndio hayo wanayoshuhudia Watanzania”.
Mara nyingi Watanzania wameshuhudia mijadala ya kejeli, malumbano, matusi, kudharauliana pale hoja zinapojengwa na upande ambao haukubaliki na upande mwingine jambo ambalo limewavunja moyo Watanzania na kutokuwa na imani ya kupata Katiba inayolenga kumlinda mwananchi.
Jukumu la wanahabari ni kutoa elimu ya kutosha kuhusu yaliyomo katika Katiba Mpya na kuandika habari za maendeleo ili majadiliano yatokanayo yawe endelevu yamtendee haki mwananchi wa kawaida kwa lengo la kuboresha maisha yao.
DSC_0077
Meza Kuu, kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Elimu, Sayansi na Mawasiliano ya Umoja wa Mataifa (UNESCO) Bw. Abdul Wahab Coulibaly, Mkurugenzi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) Bw. Ernest Sungura, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Bw. John Mongela, Mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani, Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la Tanzania (MISA-TAN), Bw. Mohamed Tibanyendera, Rais wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Bw. Kenneth Simbaya na Meneja Utafiti na Ushapishaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Bw. John Mirenyi.
“Inasikitisha kuona kuwa hali ya Mtanzania inazidi kudidimia au kubaki pale pale katika sehemu nyingi hasa vijijini katika kipindi cha miaka 40 iliyopita kwa kukosa fursa muhimu za maendeleo na viongozi hawalioni hilo”, amesema Jaji Mstaafu Mark Bomani.
Wakati huo huo mgeni huyo rasmi amekemea tabia ya kuandika habari za kuwasifu viongozi na kupokea Rushwa hali iliyojitokeza katika miaka ya hivi karibuni na kusema kwamba ni fedhea kwa tasnia ya habari kutofuata maadili ya uandishi.
Amesema kwamba nchi itaendeshwa kwa kusimamia haki na ukweli na kuwataka wanahabari wasichoke kuisimamia haki na uhuru wa nchi yao bila woga kwani bila kufanya hivyo nchi itaongozwa kiimla.
DSC_0348
Mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani, akitoa risala wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa AICC jijini Arusha mwishoni mwa juma.
“Kuna tabia ya vyombo vya habari ya vyombo vya habari kununuliwa ili visiandike au kufichua maovu ni fedhea kwani vyombo vya habari ni kioo cha jamii”.
Akizungumzia kuhusu sheria za habari za mwaka 2007 na 2008, Jaji Mstaafu amesema ni aibu kuona mswaada wa sheria ya habari umekwama kwa zaidi ya miaka 10 kwa sababu ambazo hadi leo hazijaeleweka.
Amewataka waandishi wa habari wasikate tamaa na badala yake waendelea na kupambana kuhakikisha kwamba harakati za kupata Sheria ya Haki ya Kujua inafanikiwa ili kupunguza matukio ya manyanyaso, kupigwa, kuteswa, kufungwa kwa vyombo vya habari na kuuwawa.
“Haki haiyombwi simamieni Haki zenu na songeni mbele”, ameongeza Jaji Bomani.
DSC_0429
Sehemu ya wadau wa tasnia ya Habari wakisikiliza risala ya mgeni rasmi.
DSC_0329
Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Bw. John Mongela akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa wa Arusha kwenye maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika jijini Arusha kenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC.
DSC_0112
Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la Tanzania (MISA-TAN), Bw. Mohamed Tibanyendera, akizungumza kwenye maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika kwenye ukumbi wamikutano wa Kimataifa wa AICC jijini Arusha.
DSC_0163
Wageni waalikwa na wadau wa tasnia ya habari wakiwa kwenye ukimya kumkumbuka Mwandishi aliyeuwawa mkoani Iringa Daudi Mwangosi.
DSC_0188
Mkurugenzi wa Shirika la Elimu, Sayansi na Mawasiliano ya Umoja wa Mataifa (UNESCO) Bw. Abdul Wahab Coulibaly, akitoa Ujumbe wa Pamoja wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Irina Bokovas kuhusiana na Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014.
DSC_0217
Meneja Machapisho, Utafiti na Uhifadhi Hati wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Bw. John Mirenyi, akitoa maelezo ya machapisho mbalimbali yaliyoandaliwa na baraza hilo yakiwemo yenye madhila mbalimbali yaliwahi kuwakumba baadhi ya waandishi wa habari ndani na nje ya nchi.
DSC_0241
Mkurugenzi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) Bw. Ernest Sungura, akizungumzia mchango wa mfuko huo unaowawezesha waandishi wa habari kutafuta habari za uchunguzi na zinazoigusa jamii.
DSC_0247
Wasanii wa Bendi ya Mrisho Mpoto (Mjomba Band) wakitoa burudani kwa wageni waalikwa wakati wa maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika jijini Arusha mwishoni mwa juma.
DSC_0156
Sehemu ya wadau wa tasnia ya habari wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini hapo.
DSC_0259
Katibu wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari nchini (MOAT), Henry Muhanika, akisoma hotuba kwa niaba ya Dr. Reginald Mengi kwenye maadhisho hayo.
DSC_0269
Rais wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Bw. Kenneth Simbaya, akizungumzia wakati wa maadhimisho hayo.
DSC_0286
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Absalom Kibanda, akizungumzia changamoto mbalimbali zinazowakumba waandishi wa habari wakati maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika jijini Arusha.
DSC_0288
Mkurugenzi wa TAMWA, Bi. Valerie Msoka, akizungumzia changamoto za usawa wa Kijinsia katika uongozi kwenye Vyombo vya Habari nchini.
DSC_0304
Meneja Uhusiano wa TANAPA, Pascal Shelutete, akizungumzia ushiriki wao kwenye Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 ambapo aliwataka waandishi wahabari kutumia kalamu zao vizuri katika kukuza Utalii wa Tanzania ndani na nje ya nchi.
DSC_0312
Meneja Uhusiano wa Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro, Bw. Adam Akyoo, akifafanua jambo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 ambapo amewataka waandishi wa habari kutumia nafasi yao katika kupambana na suala la Ujangili linaloendelea nchini.
DSC_0382
Mrisho Mpoto akiwafungua vitambaa wasaani wa Mjomba Bendi kama ishara ya kuwapa Uhuru waandishi wa Habari kuzungumza kilio chao mbele ya mgeni rasmi kama ujumbe wa Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014.
DSC_0398
Mrisho Mpoto na Bendi yake akighani mashairi na kuelezea madhila wayapatayo waandishi wa habari wawapo kazini ikiwemo usalama wao katika kazi zao za kila siku.
DSC_0405
Makamu wa Rais wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa habari Tanzania (UTPC), Jane Mihanji akimkaribisha mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani kuzindua Video mpya ya wimbo "Uhuru Wangu" wa Mrisho Mpoto uliokuwa kwenye Albamu yake mpya inayoitwa WAITE.
DSC_0414
Mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani, akibonyeza kitufe kuzindua rasmi wimbo huo wakati maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014.
DSC_0422
Wageni waalikwa wakitiza wimbo huo.
DSC_0466
DSC_0497
DSC_0052
DSC_0547
Mkurugenzi wa Mbeya Highlands FM, Bi. Jacqueline Mwakyambiki, akishiriki kwenye maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo Vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika jijini Arusha.
DSC_0445
Mgeni rasmi Jaji Mark Bomani akizindua Album mpya ya Mrisho Mpoto inayoitwa "WAITE".
DSC_0476
Mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani Jaji Mstaafu Mark Bomani akizindua na kuonyesha moja ya Ripoti ya Unyanyasaji dhidi ya Uhuru wa Habari iliyoandaliwa na Baraza la Habari Tanzania (MCT). Kulia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika - Taiw la Tanzania (Misa - Tan), Bw. Mohamed Tibanyendera.
DSC_0493
DSC_0518
MKUU wa Wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani, Ahmed Kipozi akiteta jambo na mmoja wa Waandishi wa Habari wakongwe Bw. Salim Salim kutoka visiwani Zanzibar.
DSC_0562
Waandishi wa Habari wakongwe (Ma-Veterans) kutoka kushoto Mama Eda Sanga, Fatuma Aloo na Leila Sheikh wakifurahi jambo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika jijini Arusha .
DSC_0359
Mshauri na Mkufunzi wa Redio Jamii kutoka UNESCO, Mama Rose Haji Mwalimu, akisalimiana na Meneja Uhusiano wa Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro, Bw. Adam Akyoo wakati maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika jijini Arusha.
DSC_0579
Wadau wa tasnia ya habari wakinunua Album ya msaanii Mrisho Mpoto.
DSC_0572
Baadhi ya wasanii wa Mjomba Band wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mwandishi wa habari mkongwe Leila Sheikh.
Share:

MATUKIO YA VIDEO

Kumbukumbu la Blogu

Recent Posts

Unordered List

Pages

Theme Support

Sample Text