Jumanne, 22 Aprili 2014

JESHI LA OKOA WATU 10

111014220509_sp_joseph_kony_304x171_afp_nocredit_27ed8.jpg

Jeshi la Uganda limesema kuwa limewaokoa watu 10 , saba kati yao wakiwa watoto, waliokuwa wametekwa nyara na wapiganaji wa kundi la waasi la LRA.
Watu hao waliokolewa katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati, ambako kundi la LRA limekuwa likiendesha harakati zake kwa miaka mingi.
Msemaji wa jeshi la Uganda, amesema kuwa kamanda mmoja wa kundi hilo Charles Okello, alikamatwa pamoja na wapiganaji wengine wanne.
Marekani imekuwa ikisaidia wanajeshi wa Muungano wa Afrika wanaomsaka kiongozi wa kundi hilo Joseph Kony kwa kuwapa ushauri na kuwasaidia na ndege wanazotumia kumsaka kiongozi huyo.Chanzo BBC, Taarifa na (A.I wa Mjengwa blog)
Wanajeshi hao hawamsaki Kony tu anayetakikana na mahakama ya kimataifa ya jinai ICC, bali wanawatafuta na viongozi wengine wakuu wa kundi hilo
Share:

0 maoni:

MATUKIO YA VIDEO

Recent Posts

Unordered List

Pages

Theme Support

Sample Text