SHEKHE wa
Mkoa wa Dodoma Mustapha Rajabu amewataka wajumbe wa Bunge Maalumu la
Katiba wanaowakilisha kupitia taasisi zao kwenye mchakato wa kuipata
Katiba mpya kutokubali kununuliwa na wawakilishi wa vyama vya siasa.
Alisema
hayo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye chakula cha pamoja kati ya
watoto yatima na wajane kilichoandaliwa na Baraza la Waislamu Tanzania
(Bakwata) kata ya Chang’ombe mjini hapa.
Alisema
wajumbe hao wanaotoka uwakilishi wa taasisi mbalimbali ndani ya Bunge
hilo wanatakiwa kutoa mawazo ambayo yatanufaisha na kuwagusa Watanzania
wote na siyo yenye mtazamo wa itikadi za kichama kama wanavyotaka
wanasiasa hao.
Kiongozi
huyo wa dini alisema wawakilishi hao wamechaguliwa kwa ajili ya
kupendekeza mahitaji yao kwenye katiba hiyo, hivyo wasikubali kununuliwa
na vyama vya siasa ambavyo vinataka kuingiza itikadi za kisiasa ndani
ya katiba.(Martha Magessa)
Pia
amelitaka Bunge hilo kutopoteza muda kwa ajili ya malumbano yasiyokuwa
na hoja muhimu ambayo yamekuwa yakiwakera watanzania ambao wanaisubiri
Katiba itakayoboresha maisha ya wananchi.
Alisema
inasikitisha kuona na kusikia kupitia vyombo vya habari wabunge hao
wakichukua muda mwingi, kukashifiana na kulumbana kwani huko ni kupoteza
muda huku wajumbe hao wakiendelea kupata posho bila kufikia maamuzi
yatakayotengeneza hiyo Katiba.
Awali
akisoma risala kwa niaba ya watoto yatima na wajane Mwenyekiti wa Baraza
hilo, kata ya Chang’ombe Salumu Mabada, aliwataka wajumbe maalumu wa
Bunge la Katiba kuendelea kuhubiri amani na upendo kwa muda wote
wanapokuwa ndani na nje ya kikao badala ya kupandikiza chuki na migogoro
na hatimaye kuleta mafarakano kwenye mchakato mzima unaoendelea wa
kuipata katiba.
Aidha
aliwataka wajumbe hao ambao miongoni mwao wanatoka taasisi za kidini,
kuendelea kumtanguliza Mungu ili amani itawale na hatima Katiba
ipatikane yenye kukubalika na watu wote.
CHANZO:HABARILEO
0 maoni:
Chapisha Maoni