
Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametahadharisha kuwa kuendelea kwa muda mrefu mapigano ya wanamgambo wanaoungwa mkono na nchi za Magharibi nchini Syria ni hatari kwa usalama wa eneo zima la Mashariki ya Kati.
Hussein Amir-Abdollahian Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia masuala ya nchi za Kiarabu na Afrika amesema mgogoro unaoendelea nchini Syria ungeweza kutatuliwa iwapo silaha na wanamgambo wanaofadhiliwa na madola ya kigeni zingezuiwa kuingia nchini humo. (J.G)
Kwa upande wake Qarqash amesema kuwa, mgogoro wa Syria hauwezi kutatuliwa kwa njia za kijeshi na kusisitiza kwamba suluhisho la kidiplomasia ndiyo njia pekee ya kutatua mgogoro huo
0 maoni:
Chapisha Maoni