Ijumaa, 4 Aprili 2014

MGOGORO WASYRIA NI TISHIO KWA MASHARIKI YA KATI


iran_38c64.png
Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametahadharisha kuwa kuendelea kwa muda mrefu mapigano ya wanamgambo wanaoungwa mkono na nchi za Magharibi nchini Syria ni hatari kwa usalama wa eneo zima la Mashariki ya Kati.
Hussein Amir-Abdollahian Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia masuala ya nchi za Kiarabu na Afrika amesema mgogoro unaoendelea nchini Syria ungeweza kutatuliwa iwapo silaha na wanamgambo wanaofadhiliwa na madola ya kigeni zingezuiwa kuingia nchini humo. (J.G)
Amir Abdollahian amesema hayo alipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Imarati Anwar Muhammad Qarqash na kuongeza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu inaamini kuwa mazungumzo na majirani zake ndiyo njia inayofaa katika kupambana na ugaidi, makundi yenye kufurutu ada na migogoro ya kikaumu katika Mashariki ya Kati.
Kwa upande wake Qarqash amesema kuwa, mgogoro wa Syria hauwezi kutatuliwa kwa njia za kijeshi na kusisitiza kwamba suluhisho la kidiplomasia ndiyo njia pekee ya kutatua mgogoro huo
Share:

0 maoni:

MATUKIO YA VIDEO

Recent Posts

Unordered List

Pages

Theme Support

Sample Text