

Skylight
Band ni Bendi ya Muziki wa Kisasa inayomilikiwa na Kampuni ya Skylight
Entertainment Limited ambayo ilianzishwa Mwaka mmoja uliopita,aina ya
muziki( wa wanaofanya Skylight ni Afropop ambayo ina mkusanyiko wa
ladha za kiafrika..
April 09 2014 wameachia wimbo wao mpya
unaoitwa Kariakoo ambapo mbali na kuachia wimbo huu mpya pia wamezindua
studio zao za kurekodi muziki zinazoitwa Skylight Studio.Skylight Studio ni studio yenye vifaa vya kiwango cha kimataifa na imetengenezwa na Studio build International(UK) ambayo ni kampuni inayofanya kazi za ujenzi wa studio ya uingeleza.
Huu ni wimbo wa kwanza kufanyika ndani ya studio za Skylight Studio ambapo Skylight pia inatarajia kuzindua hivi karibuni kituo cha mafunzo kwa ajili ya vijana wenye vipaji vya muziki yaani Skylight Academy.
Kama ni mhudhuriaji wa matamasha ya Skylight hii ni ratiba yao kwenye msimu huu wa pasaka April 20 watakua Mwanza skylight beach resort(jembe beach) pia Tarehe 27 April watakua na tamasha Maalum la kutambulisha nyimbo mpya na wanamuziki wapya hili litafanyika pale Escape One.(Awadh Ibrahim)
0 maoni:
Chapisha Maoni