
Abraham Poincheval akichunguza ndani ya Dubu wake katika makavazi ya wanyama waliowindwa na kuhifadhiwa.
Msanii mmoja nchini Ufaransa anajiandaa kulala ndani ya tumbo la Dubu
wake aliyewindwa na kuhifadhiwa katika makavazi ya wanyamapori mjini
Paris.Uamuzi wake huu umetajwa kama kuchagua kati ya maisha ya binadamu na wanyama.

Msanii huyo mfaransa anaanza maonyesho yake ya kiusanii ambayo yametajwa kuwa ya kipekee na ambayo yatashuhudia akilala ndani ya mnyama huyo kwa siku 13.
Abraham Poincheval aliyezaliwa mwaka 1972 kwa mara ya kwanza alifanya maonyesho hayo yanayojulikana kama -kuishi ndani ya ngozi ya Dubu- katika kituo cha maeonyeso ya usanii mjini Digne mwaka jana.
Sasa anajiandaa kurejelea onyesho hilo katika makavazi mjini Paris ambako atasalia ndani ya tumbo la Dubu huyo ambaye ni mnyama halisi isipokuwa tu amekaushwa na kuhifadhiwa katika makavazi hiyo.
Chanzo: BBC
(J M)
0 maoni:
Chapisha Maoni