Ijumaa, 4 Aprili 2014

MSANII KULALA NDANI YA TUMBO LA DUBU NI MAAJABU HAYA

DUBUUUU_c128c.jpg
Abraham Poincheval akichunguza ndani ya Dubu wake katika makavazi ya wanyama waliowindwa na kuhifadhiwa.
Msanii mmoja nchini Ufaransa anajiandaa kulala ndani ya tumbo la Dubu wake aliyewindwa na kuhifadhiwa katika makavazi ya wanyamapori mjini Paris.
Uamuzi wake huu umetajwa kama kuchagua kati ya maisha ya binadamu na wanyama.
DUBU2_1e666.jpg
Msanii huyo mfaransa anaanza maonyesho yake ya kiusanii ambayo yametajwa kuwa ya kipekee na ambayo yatashuhudia akilala ndani ya mnyama huyo kwa siku 13.
Abraham Poincheval aliyezaliwa mwaka 1972 kwa mara ya kwanza alifanya maonyesho hayo yanayojulikana kama -kuishi ndani ya ngozi ya Dubu- katika kituo cha maeonyeso ya usanii mjini Digne mwaka jana.
Sasa anajiandaa kurejelea onyesho hilo katika makavazi mjini Paris ambako atasalia ndani ya tumbo la Dubu huyo ambaye ni mnyama halisi isipokuwa tu amekaushwa na kuhifadhiwa katika makavazi hiyo.
Chanzo: BBC
(J M)
Share:

0 maoni:

MATUKIO YA VIDEO

Recent Posts

Unordered List

Pages

Theme Support

Sample Text