Jumanne, 24 Juni 2014

IKIWA NI MASAA24 YALIYOPITA YA YULE MWANAMKE WA SUDAN AKAMATWA TENA

mwanamkeSiku moja baada ya kuachiwa huru kwa yule mwanamke aliyekuwa amehukumiwa kifo kwa kosa la kuolewa na mwanaume wa kikristo,Taarifa kutoka nchini Sudan zinasema kuwa mwanamke huyo amekamatwa tena.
familiaJina lake ni Meriam Ibrahim,alikamatwa akiwa na familia yake katika uwanja wa ndege mjini Khartoum,watu waliomkamata walikuwa wamevalia mavazi ya kiraia ingawa wanaaminika kuwa ni wanajeshi wa Serikali.
Duru zinasema kuwa Meriam Ibrahim aliyejifungulia jela alikuwa anajiandaa kuondoka nchini Sudan pamoja na familia yake mpaka sasa haijajulikana kwa nini alikamatwa na karibu watu arobaini waliokuwa wamavalia mavazi ya kiraia siku moja tu baada ya kuachiliwa kuambatana na uamuzi wa mahakama ya rufaa.
Meriam alikamatwa mara ya kwanza mwezi Februari na kujifungulia mtoto wake wakike akiwa jela baada ya kuhukumiwa.
Share:

0 maoni:

MATUKIO YA VIDEO

Kumbukumbu la Blogu

Recent Posts

Unordered List

Pages

Theme Support

Sample Text