• This is default featured slide 1 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

  • This is default featured slide 2 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

  • This is default featured slide 3 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

  • This is default featured slide 4 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

  • This is default featured slide 5 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by NewBloggerThemes.com.

Alhamisi, 30 Oktoba 2014

PICHA NNE ZA CHIDI BENZI BAADA YA KUPATA DHAMANA HAPO JANA MAHAKAMANI.

chidi 3Alishikiliwa na Polisi baada ya kukutwa na dawa za kulevya kwenye uwanja wa ndege Dar es salaam wakati akijiandaa kupanda ndege kwenda Mbeya kwenye show.
Baada ya kufikishwa Mahakamani October 28 2014 na kusomewa mashtaka matatu alirudishwa rumande huku kesi yake ikiahirishwa mpaka November 11 2014 na wakati huohuo pia ikisemekana alikua kwenye mipango ya kupata dhamana.
October 29 2014 Chidi Benz alipata dhamana kwenye Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu baada ya kupata Wadhamini wawili pamoja na shilingi milioni moja.
chidi 4
Chidi 2
Chidi 1                                      PICHA NA MILLARDAYO.COM
Share:

UCHUNGU WA WAZAZI HAWA KWA WATOTO WAO UMEFIKIA KIWANGO HIKI......

Wazazi Kulinda ShuleKuna ukweli kwenye msemo wa waswahili unaosema “uchungu wa mwana aujuaye mzazi”, na ndio maana stori nnayokuletea huenda ikawa ngeni na hujawahi kukutana nayo, lakini wazazi hawa wameonesha namna walivyo na uchungu kwa vitendo na sio maneno pekee.
Stori kutoka Kenya inahusu kitendo cha wazazi kuamua kujichukulia jukumu la ulinzi wa eneo la shule ili kukabiliana na vitendo vya uhalifu ambavyo vimekuwa vinajitokeza mara kwa mara katika maeneo hayo.
Kila jioni Esuruan Awet ni moja ya wazazi hao ambao hujiunga na kikundi cha askari Polisi wa akiba kwa lengo la kupiga doria eneo la shule ya msingi Nakatong’wa, Mashariki mwa Turkana huko Kenya.
Eneo la shule hiyo limekuwa likikabiliwa na matukio ya kuvamiwa mara kwa mara kitendo kilichowafanya wazazi hao kujiunga na kikosi hicho kukabiliana na uhalifu huo.
Share:

SEKUNDE 90 ZA RAPPER CHID BENZI..............

AyoTV 12
 Ayo Tv iliweza kumnasa rapper huyu na kuzungumza naye mawili matatu hebu sikiliza hapa na kuona.Rapper Chidi Benz ameachiwa kwa dhamana na Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu Dar es salaam baada ya kutimiza masharti ambayo ni pamoja na kupeleka Wadhamini wawili na shilingi milioni moja za Kitanzania ikiwa ni kutokana na kukamatwa na dawa za kulevya kwenye uwanja wa ndege Dar akisafiri kwa Fastjet kuelekea Mbeya.

Bonyeza hapa kwa kusikiliza:

Share:

Jumatano, 29 Oktoba 2014

ZAMBIA WAMPOTEZA RAIS WA PILI AKIWA MADARAKANI.

Sata II
Aliyekuwa rais wa Zambia Michael Sata amefariki usiku wa jana tarehe 28 Oktoba kutokana na ugonjwa ambao bado serikali ya nchi hiyo haijaweka wazi.
Sata (77) amefariki akiwa anatibiwa nchini Uingereza alikokuwa amelazwa kwa zaidi ya mwezi mmoja.
Rais huyo amefariki siku 4 baada ya nchi hiyo kusherehekea madhimisho ya miaka 50 tangu ipate uhuru, ambapo kutokana na kuwepo nje ya nchi akipata matibabu hakuhudhuria sherehe za maadhimisho hayo.
Rais Sata ambaye amekuwa maarufu kwa jina la ‘King Cobra‘ amekaa madarakani kwa takribani miaka 3 tangu achaguliwe kushika wadhifa huo mwaka 2011, ambapo anakuwa rais wa 2 kufariki akiwa madarakani nchini humo baada ya Levy Mwanawasa, aliyefariki mwaka 2008.
Share:

STORI KUBWA SITA ZA LEO KWENYE MAGAZETI MBALIMBALI.

Hot News II
MTANZANIA
Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe limewafukuza kazi askari polisi watatu kwa kosa la kupigana hadharani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Fulgence Ngonyani alisema kuwa askari hao walitimuliwa kazi baada ya kupatikana na hatia kwa kukiuka taratibu za kazi zao.
Alisema askari hao walipigana hadharani saa10 alasiri na jeshi kuamua kutoa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwa watumishi wenye tabia ya kupigana hadharani.
MTANZANIA
Jeshi la Polisi Mkoani Kagera limetumia mabomu ya machozi kuwatawanya wanachama waliojitokeza kumpokea Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la wanawake wa Chadema (BAWACHA) Halima Mdee.
Walilazimika kutumia mabomu ya machozi wakati Mdee alipokwenda kusaini kitabu cha wageni kwenye ofisi za Chama hicho.
Mbali na kutumia mabomu ya machozi pia Jeshi hilo limezuia mikutano yote ya hadhara iliyokua ihutubiwe na Mdee jana kwa madai kuwa hakutakua na usalama wa kutosha.
MWANANCHI
Uongozi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili umesema umepandisha gharama za huduma ya kitanda na chakula ili kuongeza mapato yakatayosaidia kulipa deni la bohari kuu ya dawa MSD
Kauli hiyo ya meneja uhusiano Muhimbili Aminiel Algaesh imekuja siku moja baada ya hospitali hiyo kupandisha gharama na kusema gharama hizo zitasaidia kupunguza deni la bilioni8 wanazodaiwa na MSD.
Alisema baada ya kupitia utaratibi huo ambao ulianzishwa mwaka2003 uongozi uliadhimiai kupanda kwa gharama za utoaji huduma za chakula na malazi  hivyo kulazimika kubadilisha mfumo  na kumtaka mgonjwa anayelazwa kuchangia5000 kwa siku na chakula2000.
MWANANCHI
Hatimaye mwili wa Rosemary Marandu uliohifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti hospitali ya KCMC Moshi kwa siku53 umezikwa huku maziko yake yakigubikwa na utata na kuhudhuriwa na wanaume sita.
Mazishi hayo yalifanyika juzi katika makaburi na Karanga  na hakuna aliyehudhuria kati ya baba na mama wa marehemu huku walomzika kutumia muda mfupi sana kumaliza zoezi la kumzika.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema waliona magari mawili moja likiwa na mwili wa marehemu yakiingia makaburini hapo lakini utata umezidi hukusu ni nani aliyefanya maziko hayo baada ya ndugu wote kususia.
UHURU
Kila Mtanzania nchini atakua na uwezo wa kupata simu za kisasa na yenye uwezo mkubwa (Smartphone) kwa bei ya chini kabisa katika miaka mitano ijayo kuanzia mwaka2020.
Hiyo ni moja ya mipango ya kampuni mpya ya simu inayojiandaa kuingia katika soko la simu Tanzania.
Kampuni hiyo pia imemwambia Rais Kikwete kuwa itasambaza mawasiliano ya Internet kwa kila kijiji nchini na kwamba kwa taasisi za umma kama vile shule,hospitali na vituo vya polisi zitapatiwa huduma hiyo bila malipo yoyote.
Mwenyekiti wa kampuni hiyo ya Viettel toka Vietnam Nguyen Munh amemwambia Rias Kikwete kuwa  kampuni hiyo inakusudia kumwezesha kla Mtanzania  kumiliki simu hizo kwa punguzo kubwa na pia kupunguza huduma za Internet.
UHURU
Muunganiko wa vyama vinne vya upinzania umeendelea kupokelewa kwa hisia tofauti huku wengine wakiuponda ambapo Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe amesema muungano huo hauna tija kwa Taifa.
Zitto alisema Muunganiko huo ni kwa ajili ya wasaka utawala badala ya uongozi ambao pia wanaweza kuitwa wasaka tonge kwa kutaka kujinufaisha binafsi.
Zitto alisema katika maeneo mbalimbali nchini ,mazao ya wakulima kama mahindi na mpunga yamekua yakiharibika kutokana na kukosekana kwa masoko hivyo kuendelea kuwa maskini.
Share:

UCHUNGUZI WAENDELEA KUHUSU YA KITU KILICHOJULIKANA KAMA BOMU DAR ES SALAAM.

Breaking nEWS IIII

    Taarifa iliyoripotiwa na kituo cha Radio One imesema kuwa hofu imetanda eneo la Kijitonyama Dar es Salaam karibu na kanisa la KKKT baada ya kuonekana kwa kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu, na kwa mujibu wa taarifa hiyo jeshi la polisi tayari wamefika eneo la tukio na kuweka ulinzi eneo la tukio kwa sababu za kiusalama.
Share:

Jumatano, 22 Oktoba 2014

AKON AKIWA NA D'BANJI KWENYE COLLABLE LA HATARI..............


Akon and D'banj have collaborated in two songs., one titled 'Frosh' and the other titled 'Feeling A Nigga'. The videos for Akon's Frosh was shot in Atlanta yesterday. Both songs will be dropped before Christmas



Share:

Jumanne, 21 Oktoba 2014

UMEISIKIA HII KUWA EBOLA YAPATA CHANJO .........................................

Ebola NewShirika la afya duniani, WHO limearifu kuwa liko mbioni kufanya majaribio ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa Ebola, ambao umeripotiwa kuua takribani watu 4,500 huku nchi za Afrika Magharibi zikiripotiwa kuathirika zaidi tangu kulipuka kwa ugonjwa huo.
Taarifa iliyoripotiwa na CNN imesema kuwa shirika hilo limepanga kuanza utekelezaji wa jaribio hilo mapema Januari mwaka 2015 katika nchi za Afrika Magharibi, huku wakisisitiza kuwa chanjo zote hazina madhara kwa afya ya binadamu, japo chanjo hiyo haitowahusu wagonjwa ambao tayari wana maambukizi Ebola.
Mratibu wa zoezi hilo Dk. Marie Paule Kieny amesema, chanjo hiyo itatolewa kwa mtu yoyote atakayekuwa tayari kujitolea kushiriki.
Amezitaja nchi za Mali, Uingereza na Marekani kuwa ni baadhi ya nchi ambazo jaribio la chanjo hiyo litafanyika.
Shirika la afya limesema limeagiza wataalamu kufanya ziara Afrika Magharibi katika nchi ambazo wananchi wake wameathirika zaidi na ugonjwa huo, ambapo pia ziara hiyo itahusisha pia zoezi la ukaguzi wa vituo ambavyo vitatumika kutolea huduma hiyo ya chanjo.
Iwapo chanjo hii itafanikiwa itafufua matumaini kwa watu wa Afrika ya Magharibi ambao wameshuhudia athari kubwa zilizosababishwa na Ebola ambapo watu zaidi ya 4,500 wameripotiwa kufariki na wengine zaidi ya 9,000 wana maambukizi ya ugonjwa huo.
Share:

BAADA YA BASI NENDA SASA MO MUSIC AMEKUJA KIVINGINE..........

mooooHit maker wa single ya Basi Nenda kutoka 88.1 Mwanza Mo Music leo ameachia single yake mpya baada ya Basi Nenda kufanya vizuri,hii kaifanya Mazuu Records chini ya Producer Mazuu.
mo
BONYEZA HAPA KUSIKILIZA:


Share:

MSIBA MWINGINE BAADA YA YP TUMEONDOKEWA NA MWIGIZAJI MWINGINE......SOMA HAPA ...

SherryNi masaa machache tu yamepita tangu muziki wa kizazi kipya Tanzania, Bongo Fleva kumpoteza aliyekuwa staa wa muziki huo kutoka kundi la TMK Wanaume Family, aliyekuwa akifahamika kwa jina la YP, taarifa nyingine ya simanzi inahusu msiba wa aliyekuwa muigizaji wa Bongo Muvi.
Katika ukurasa wake wa instagram, muigizaji na mchekeshaji maarufu anayefahamika kwa jina la Kitale ama Mkude Simba (@mkudesimbaoriginal), amepost picha ya muigizajiShery Mwana aliyefariki masaa machache yaliyopita.
Kwa mujibu wa Kitale, muigizaji huyo mbaye jina lake halisi ni Sherry Charles Magali, aliwahi kushiriki na Kitale katika movie mbali mbali ikiwemo Kipotabo na Nyumba Nne.
Sherry II
Share:

BREAKING NEWS:KIPINDI CHA INTERVIEW DAY SASA KIMEANZA KURUSHA MATANGAZO YAKE RASMI......SOMA HAPA ZAIDI...

KILE KIPINDI CHA INTERVIEW DAY SASA KIMEANZA MATANGAZO YAKE RASMI TOKA JANA,
UKITAKA KUYAPATA WAWEZA KUKIONA ONLINE SASA KUPITIA ACCOUNT YA YOUTUBE: EMMANUELI ELIAS.
WAWEZA KUJIFUNZA MENGI JUU YA KIPINDI HIKI KARIBU SANA KUWA MDAU WA KIPINDI HIKI NA MAONI YAKO NI MUHIMU KWETU ILI TUWEZE KUKIBORESHA KIPINDI HIKI.

Share:

NI PICHA 11 KUTOKA KEKO, NYUMBANI KWENYE MSIBA WA MSANII WA TMK YP

YP IIIAliyekuwa msanii wa muziki wa Bongo Fleva, YP ambaye amefariki usiku wa jana katika hospitali ya Temeke wakati alipokuwa akitibiwa maradhi ya kifua kikuu (TB) anatarajiwa kuzikwa siku ya kesho katika makaburi ya Chang’ombe jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa ndugu wa marehemu, YP ambaye jina lake halisi ni Yessaya Ambilikile ameugua kwa kipindi cha takribani miezi 2 kabla ya kufikwa na umauti hapo jana.
Hizi ni picha 11 za kutoka eneo la Keko, nyumbani alikokuwa akiishi msanii marehemu ambapo taratibu za mazishi zinafanyika.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
CHANZO CHA PICHA :MILLARDAYO.COM
.
Share:

CHAGUA KING WAKO WA BONGO FLEVA KATI YA HAWA...................................................

HAPA NI FULL UTATA JE YUPI ANAKUFAA KUWA KING WAKO WA BONGO FLEVA.................
Share:

KILICHOMTOKEA AISHA BU,CHAMTOKEA BATULI PIA, AFUNGUKA KWA MASIKITIKO SOMA HAPA.......

Batuli
Habari mpya magazetini leo ni kuhusu muigizaji wa filamu nchini Aisha Bui kufanya vurugu ofisi za YUNEDA ambayo ni kampuni ya usambazaji wa filamu nchini kwa mdai ya kutomlipa aisha Bui
pesa yake kwa wakati na kumlipa nusu licha ya Aisha kusubiri kwa muda mrefu bila mafanikio huku mhusika akidaiwa kum-block Bui katika simu yake ndipo hasira zikampanda Aisha na kufunga kibwebwe mpaka ofisi hizo zilizopo Mbagala na kukinukisha. Batuli Yobnesh Yusuph nae amefunguka baada ya sakata hilo na kusema hata yeye yameshamtokea hayo kutokana na baadhi ya wasambazaji wasivyo waaminifu kutaka kuwadhulumu wasanii. Batuli ameandika.........

"Haya ndio tunayokutana nayo wasanii wa kike, Kiukweli kabisa wapo watu wanaoturudisha nyuma kila kukicha, Mbaya zaidi wanaofanya hivi ni wale wanaoheshimika kwenye jamii na sio kwamba hana uwezo wa kukulipa bali hufanya hivi kukukomoa tu, Binafsi nina maumivu kama ya @aishabuithebootybaby unafanya kazi na mtu kwa makubaliano fulani tena kwenye mazingira magumu matokeo yake mwisho wa siku anakudhulumu haji yako, Ukitupia picha mitandaoni unakutana na maswali kutoka kwa mashabiki "Tumekumic Hatukuoni Kwenye Movie Siku Hizi" Mazingira ya Ubabe, Dhulma, ndivyo vinavyotawala kwenye fani hii, Haipendezi na sio vyema kwa wale wenye tabia kama hizi, Acheni dhulma kwenye kazi, Mkumbuke tunaaga kwenye familia zetu kuwa tunakwenda kazini, Matokeo yake ukirudi nyumbani watu wanakushangaa badala ya kuhudumia familia wewe ndio unakuwa Matonya. Kesho na kesho kutwa unaandikwa magazetini unagombeae bwana watu wanakuona muhuni sasa kwa style hii ya kudhulumiana unategema mtu ajikimboe kwa njia gani?"
Share:

HAYA SASA UMEIPATA HII, KIMENUKA KWA MISS TANZANIA 2014....SOMA HAPA

Baada ya watanzania na wadau wengi wa urembo na mitindo nchini kukinukisha kwa kuukataa ushindi wa Sitti Mtemvu kuvikwa taji la Miss Tanzania 2014 kwa madai hakuwa na sifa na ana umri mkubwa sasa kimenuka !...
Habari ambazo zimeandikwa leo mpaka magazetini ni kuwa kuna uwezekano mkubwa wa Sitti kuvuliwa taji la Miss Tanzania 2014 huku issue ya umri wake ikiwa moja ya point kuu za kumvua taji hilo. Inadaiwa pia kuwa kwasasa wajumbe wa kamati ya Miss Tanzania wamegawanyika ambapo kuna wasioukubali ushindi wa Sitti huku wengine wakiona sawa tu.


Habari zaidi zinadai kuwa kamati na waandaaji wa Miss Tanzania wanataka kumvua Sitti taji ili kuendelea kuweka taswira, imani na usafi wa shindano hilo kwa kuondoa kashfa ya upendeleo na rushwa kama ilivyo midomoni mwa watu kuhusu shindano hilo kwasasa baada ya Sitti kukataliwa kuwa Miss Tanzania 2014. Pia inadaiwa kuwa kamati ya Miss Tanzania ina hofu na issue ya Sitti kufika kwa waandaaji wa Miss World na hivyo kuweza kulizuia shindano la Miss Tanzania miaka kadhaa au kufuta ushiriki wao kabisa.

Inadaiwa zaidi kuwa ikiwa Sitti atavuliwa taji basi kuna uwezekano mkubwa Jihan Dimachk akaiwakilisha Tanzania katika shindano la Miss World 2015 kutokana na watanzania wengi kumkubali na kudai ameonewa kuliko hata mshindi wa pili Lilian Kamazima.

Vigezo vinavyolalamikiwa kumpa ushindi Sitti ni utata wa umri wake huku wazazi wake mama akisema mwanae ana miaka 29 wakati baba mzazi na Sitti mwenyewe wakisema ana mika 18 huku passport yake ikionyesha ana miaka 25, umbo lake anadaiwa kuwa mnene hivyo kukosa sifa za umiss, anadaiwa kuwa na mtoto wa miaka 6-8, swali hakujibu vizuri huku akichanganya na lugha ya kifaransa ambayo awali hakuichagua, inadaiwa kuwa sifa zake hazikumzidi Jihan na Lilian Kmazima walioshika nafasi za pili na tatu.

Jihan

Jihan Dimachk ambaye watanzania na mashabiki wengi wa urembo wamelalamikia kuwa ameonewa yaani yeye ndiye alistahili kupewa taji la Miss Tanzania 2014
Share:

SHABBY ANGEL NA BOB JUNIOR WAANGUKIA KWENYE DIMBWI ZITO LA MAHABA......

Mahaba niue !....Gossip mpya ni kuwa actress anayekuja juu kwa kasi kama moto wa kifuu  Sabby Angel ambaye pia ni mwanamuziki wa kizazi kipya tayari anadaiwa kuwa kwenye dimbwi zito la mahaba na Bob Junior ambaye pia ni star wa Bongofleva na mmiliki wa Sharobaro Records.
Kwa mujibu wa chanzo makini toka kwa wawili hao kikizungumza na Swahiliworldplanet  jioni hii kimesema kuwa Sabby na Bob Junior wanapendana na mahaba yao yalianzia studio ya Bob Junior hivi juzi kati Sabby alipoenda kwa ajili ya issue zake za muziki ndio kila mmoja akamzimikia mwenzake.

Ukiachilia mbali hayo Bob Junior amekuwa akirusha comments na kuchat kimahaba na Sabby Angel kwenye mitandao ya kijamii hususani Instagram kama inavyoonekana hapo chini.


Hapo Sabby aliweka picha ya Bob Junior na Bob Junior kuanza kuchombeza
Bob Junior hivi karibuni aliachia wimbo wake mpya wakati Sabby kwasasa anatamba sokoni na filamu ya Siri Ya Giningi huku filamu yake mpya ya Moto Wa Radi ikitarajiwa kuingia sokoni muda si mrefu kuanzia sasa.
Share:

UNAFAHAMU KUHUSU OSCAR PISTORIUS? ISOME HAPA!!!!!!!

PistoriusMwanariadha wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius(27) ambaye amekutwa na kesi ya bila kukusudia yuko katika wakati mgumu baada ya kukutwa na hatia ya mauaji.
Kutokana na kukutwa na hatia ya kuua bila kukusudia mwishoni mwa wiki iliyopita, masaa machache kuanzia sasa, ndani ya mahakama ya the Palace of Justice iliyopo jijini Pretoria, Pistorious atasomewa hukumu.
Hukumu ambayo Pistorious atakabiliana nayo huenda ikawa kifungo kisichozidi miaka 15 jela, kulipa faini, ama kifungo maalum chini ya idara ya urekebishaji wa tabia, ambapo atakuwa akifanya shughuli za kijamii, au kifungo cha nje.
WWW.SAMERICK.BLOGSPOT.COM Itaendelea kukuhabarisha kwa lolote litakalo jitokeza kwa kina na wakati maalum.....
Share:

UNAIJUA ZAWADI ALIYOPEWA T.I NA BOSS WA CLOUDS.......? ISOME HAPA

Untitled33
Mfalme wa Kusini,Clifford Joseph Harris, Jr aka T.I baada ya kuacha historia kubwa Tanzania katika Tamasha la Serengeti Fiesta 2014 Oct 18 Leaders Club Dar es Salaam, Mkurungenzi Mtendaji wa Clouds Media Group,’Joseph Kusaga’ alimkabidhi msanii huyo zawadi  yenye mfano wa silaha za jadi.
.
.
Itazame  video hapa mtu wangu uone jinsi alivyokabidhiwa zawadi hiyo

       CHANZO CHA PICHA NA:MILLARDAYO.COM
Share:

BREAKING NEWS:UMESIKIA HII KUTOKA MAREKANI EBOLA YAWA TISHIO HUKO?

CNN EbolaNi kawaida kusikia mtu kapewa ‘a.k.a’ ambayo lazima kuna kitu kilichopelekea akapewa a.k.a hiyo, huenda ikawa ni muonekano wake, tabia, mavazi ama kitu chochote kile kinachohusiana na yeye.
Watu wamekuwa wakitoa ‘a.k.a’ hata kwa vitu vingine pia, lakini kali ni hii kutoka Marekani, ambapo ripota wa kituo cha televisheni cha CNN alitoka kali baada ya kutoa a.k.a ya ugonjwa wa Ebola, kwa kuuita “Fear-bola”
Mel Robbins- Fear-bolaMel Robbins amenukuliwa katika ukurasa wa mtandaoni wa kituo hicho akisema; “Fear-bola inashambulia sehemu ya ubongo inayohusika na kuwaza mambo ya busara”
Mtangazaji huyo aliongezea kuwa ‘Fear-bola’ ilianza pale ilipogundulika wauguzi 2 walipata maambukizi hayo huko Dallas, na baadaye ikatanda ‘ugonjwa wa hofu’ kila kona ya Marekani.
Share:

PATA NAFASI NA DAKIKA 3 ZA UKWELI KUCHEKI KICHUPA HIKI SAFI KUTOKA KWA PHD................

HMD 2Gelly wa Rhymes na Hemedy PHD wamekua friends ambao kazi yao kubwa ya movie wanaifanya pamoja lakini kazi yao nyingine ikibaki palepale ambayo ni kufanya muziki wa bongofleva.
Ninayo furaha sasa hivi kushare na wewe video yao mpya inaitwa ‘The One


Share:

BREAKING NEWS: HII NI KUTOKA KWA VANESSA MDEE KUWA TUSUBIRIE KICHUPA CHAKE KINGINE KUTOKA NJE YA TANZANIA

V 1Maoni ya Wasanii wengi wakubwa wa Tanzania niliozungumza nao kwa asilimia kubwa hayapingani na maamuzi ya mastaa wengi wa bongo kwenda kufanya video za muziki wao nje ya Tanzania na hii ni sababu ya kuutafuta ubora wa kuiuza vizuri bidhaa yao.
Miongoni mwa wasanii waliozungumza na Fid Q ambae anasema kwa kutolea mfano mdogo kwamba Tanzania ina warembo wazuri sana wa kutokea kwenye video lakini huwa hawakubali sababu wanaona ni kujishushia hadhi, kingine ni Madirector kutaka kufanya wanavyojua wao na hawawapi Wasanii nafasi ya kueleza wanatakaje.
Baada ya kukupa hayo, taarifa ikufikie kwamba mwimbaji staa wa hit single ya ‘hawajui‘ Vanessa Mdee amesafiri kwenda nje ya Tanzania kwa ajili ya kufanya video ya hiyo single ambapo aliiweka hiyo picha hapo juu kwenye instagram yake na kuandika hii caption hapa chini akiwa uwanja wa ndege Dar es salaam.
V 2Kaenda nchi gani? anaifanya na nani? mengine ya ziada unataka kuyajua? kaa karibu na samerick.blogspot.com mtu wangu pia jiunge na mimi kwenye twitterfacebook na instagram ili kikitokea chochote tu nikudondoshee.

Share:

KURASA ZA MBELE NA MWISHO ZA MAGAZETI YA LEO PITIA HAPA........................................

.
.
Kama kawaida samerick.blogspot.com inakupa vichwa vya habari vya magazeti yote ya kila siku. Leo pia kuna headline mpya kwenye magazeti mbalimbali. Chukua muda wako kupitia kila kilichoandikwa kwenye kurasa za mbele za magazeti ya leo.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Share:

MATUKIO YA VIDEO

Kumbukumbu la Blogu

Recent Posts

Unordered List

Pages

Theme Support

Sample Text