Jumatatu, 13 Oktoba 2014

INTERVIEW DAY:KUKATA TAMAA SI JAMBO ZURI HATA KIDOGO KWENYE MAISHA YA KILA SIKU HEBU PATA HII....


Mathias Canal akiwa amepanga msitari na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Igowole kwa ajili ya kwenda kuchukua chakula
Wanafunzi hao wakimsikiliza Mathias Canal
Wengine husoma habari zetu, wengine hutusikiliza hivyo wanapopata nafasi ya kuonana na wanaowasona au kuwasikiliza hakika hufurahi.
Pichani ni wanafunzi wa kidato cha tano shule ya sekondari Igowole iliyopo Wilayani Mufindi, Mkoa wa Iringa.Shule ambayo imeongoza kitaifa matokeo ya kidato cha sita mwaka huu, Nimezungumza nao kuhusu mambo mbalimbali yahusuyo elimu lakini pia tasnia ya habari.
Nilipanga mstari wa kupata chai ya bila kitafunwa, kwani kitafunwa kila mtu hujitegemea, nilifurahi sana maisha yale kwani yalinikumbusha miaka kadhaa iliyopita nikiwa kidato cha tatu Nsumba Boys Jijini Mwanza kwani tulikuwa na mlo mzuri asubuhi kwa kupata chai na skonzi 2 kila mwanafunzi.(P.T)
Walifurahishwa na maelezo juu ya umuhimu wa habari lakini pia ugumu wa kutafuta habari.
Hakika wanafunzi hawa wameniuliza maswali mengi hususani katika mauaji ya Mwanahabari Daud Mwangosi aliyeuwawa Sept 2012 akiwa kazini kijiji cha Nyololo.
Wengine walisema wanaogopa kuwa waandishi kwa kuhofia kupigwa na polisi.Ila niliwatia moyo kwamba kila kazi ina changamoto zake, hivyo wasikate tamaa na kuziamini ndoto zao ile zitimie.
Share:

0 maoni:

MATUKIO YA VIDEO

Kumbukumbu la Blogu

Recent Posts

Unordered List

Pages

Theme Support

Sample Text