
Wanasayansi kutoka Taasisi ya Afya Ifakara ‘IHI’ wamegundua mradi wa kutengeneza vyandarua kwa kutumia manyoya ya kuku yaliyorundikwa nyumbani na majalalani ikiwa ni moja ya jitihada za kuendeleza vita dhidi ya ugonjwa wa malaria hasa kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.
Kwa mujibu wa taarifa ya utafiti wa kila mwezi iliyotolewa na Taasisi hiyo kwenye Gazeti la NIPASHE,manyayo hayo yatakua yanakusanywa kutoka maeneo ya masoko na kwenye makazi ya watu.
Kukamilika kwa mradi huo wa ubunifu utakua ni sehemu ya kupunguza takataka zinazotokana na mlundikano wa manyoya yaliyozagaa maeneo mbalimbali na kukabiliana na ugonjwa wa malaria ambao ni hatari kwa afya za wengi.
Wataalam wa afya wanaeleza kuwa vyandarua vimethibitishwa kuwa na uwezo wa kumkinga mtu dhidi ya maambukizi ya malaria lakini familia nyingi bado hazina uwezo wa kuzinunua.

Mbali na kusaidia kukabiliana na malaria,mradi huo pia utaleta matokeo chanya katika utunzaji na kuibua fursa nyingi za kibiashara.
Utafiti huo ulifanywa na DK.Samson Kiware na Isaac Lyatuu kutoka Taasisi hiyo kwa ufadhili wa Grand Challenge Canada.
0 maoni:
Chapisha Maoni