
Baada ya kocha wa Manchester United Van Gaal kusema Wellbeck hakuweza kufunga mabao ya kutosha wakati alipokuwa Old Trafford, mchezaji mstaafu Allan Shearer amesema Danny Welbeck ambaye ni mshambuliaji mpya wa Arsenal anaweza kufunga mabao hata 25 kwa msimu mmoja akipewa nafasi. Shearer akihojiwa na Radio 5 alisema hakubaliani na kauli ya kuwa Wellbeck hawezi kufunga magoli 20 au 25 kwa msimu mmoja,ataonyesha uwezo wake Arsenal.
Wellbeck mwenye umri wa miaka 23 alijiunga na kikosi cha The Gunners kutoka Manchester United kwa kwa ada ya pauni millioni 16 katika siku ya mwisho ya dirisha la usajili barani ulaya.
0 maoni:
Chapisha Maoni